Monday 17 August 2009

WIKI IMEANZA: Nawatakieni wiki njema.

Tunataka kuvuka ng'ambo tuwahi kazini na kwenye mihangaiko mingine ya Jijini. Lakini swali ni kwamba tutaenea wote kweli.Hizi ni nyakati za MV.Alina.
Kwa sasa tunaipongeza Serikali kwa kutuimarishia usafiri kiasi fulani kwa hii MV.Magogoni ambayo ina uwezo mkubwa tofauti na ile Mv.Alina. Hata hivyo kauli yetu na ombi letu ni kwa Serikali kujitahidi kuweka Daraja la kuunganishi sehemu hizi mbili maana hiyo itasaidia sana suala zima la usafiri na maendeleo pande zote.Maana hata maembe ya "Kibada" yatafika kiurahisi sokoni Kariakoo.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako