Thursday 6 December 2012

TUWAKUMBUKE NA WATOTO HAWA

Tunapokuwa katika harakati za kuboresha maisha na kuinua kipato, tukijaaliwa na mola tukumbuke katika matumizi yetu na matendo yetu ya kila siku kuwa kuna watoto wengine wanatafuta elimu kwa kusomea chemli, kuna wanaoenda shuleni nguo zimechania na hawana njia mbadala ya kujikwamua.




Wednesday 5 December 2012

WIZI MTUPU


Picha hii inanikumbusha ule ujanja wa mbuni kuchimbia kichwa chacke kwenye kichaka huku mwili wote upo nje kana kwamba anajificha. Huyu jamaa ni vyema akaenda kijijini kulima matembele kulikoni kuendelea na usanii huo maana siku wajanja kama mie tukimgundua, ni kichapo cha mbwa mwizi.  Kipofu anasoma message,anaandika title tena kwa kiingereza, wapi na wapi?




UBUNIFU/KUIGA

Baada ya kuiona picha ya ubunifu wa michezo ya watoto, warembo hawa nao wakatengeneza yao

Tuesday 4 December 2012

VIPAJI TULIVYONAVYO BINADAMU

Hii ni live, dada Angel alipotembelea Mbuga za wanyama Afrika ya Kusini. Hapa ni sehemu wanapoita "Lion Encounter"


SIO TISHIO, NI MANENO YAGUSAYO


UTAFUTAJI WA KIMASHA MASHAKA


Hii inanikumbusha msemo "Punda afe mzigo ufike", Ni kweli tunapaswa kujitahidi kutafuta, lakini ni kwa namna gani tunatafuta na tunanufaika vipi na utafutaji huo. Mwisho wa siku upakiaji huu wa bidhaa hii kwenye hili gari wahatarisha maisha na uharibifu zaidi kuliko faida ipatikanayo.





UJUMBE WA LEO

Ndege anapokuwa hai huwa anakula sana funza, lakini atakapokufa funza humla yeye. 
Maisha hubadilika kila wakati hivyo usimdharau wala kumuumiza mtu yeyote katika maisha. 
Unaweza kuwa imara saaana leo lakini kumbuka maisha ni imara kuliko wewe. 
Mti mmoja unaweza ukatengeneza mamilioni ya njiti za kiberiti lakini muda ukifika njiti moja tu ya kiberiti inaweza ikachoma msitu mzima.
Kuwa mwema kwa kila mtu.



Monday 3 December 2012

MTOTO UMLEAVYO - 1




WIKI IMEANZA

Pilika pilika za maisha zimeanza tena. Ni mwanzo wa wiki, nami nawatakia wadua kila la kheri katika uchacharikaji wa kufanya maisha kuwa bora zaidi.




Sunday 2 December 2012

SIDHANI KAMA INASAIDIA


Jana tulikuwa tunaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani, nikamwona huyu jamaa yangu na kujiuliza kama hii ndo gear ya kuzuia maambukizi, basi hapa atakuwa mbali na ukweli au unasemaje mdau. Samahani kwa picha hii kama itakukwaza lakini ni kufikisha ujumbe tu.



ASUBUHI NJEMA

Mwaka unapokaribia ukingoni tunalazimika kutathmini mafanikio na vikwazo vya maendelea. Lakini kwakuwa bado tuna mwezi mmoja si vibaya kujitahidi pale ambapo bado juhudi haijawa ya kutosha.

Wednesday 21 November 2012

Saturday 10 November 2012

Sunday 28 October 2012

Wednesday 24 October 2012

ULINZI MKALI

 Kutokana na dunia ya leo ilivyo, kwa sasa kila kitu chahitaji ulinzi, Mali zahitaji kulindwa, afya nazo zahitaji kutunzwa. Hapa twaona swahiba kaamua kufunga ndala zake kwa kofuli ili kuzilinda. Lakini ni kweli amezipa usalama sahihi???? Hiyo yatosha watu kutoziiba au hata atakayeziiba kushindwa kuzitumia kwani????

Na ujumbe mwingine wahusisha ulinzi wa afya zetu.

Tuesday 23 October 2012

ULISHAWAHI KUKUTANA NA HII...........


HAPPY BIRTHDAY NICKY

Tumia kifaa hiki kutambua Birthday Party inafanyikia wapi? Hakuna kiingilio

Wadau, leo ni "bethdei" yangu. Napenda kuwashukuru nyote kwa fadhila za kila namna, furaha mlizonipatia hadi nikaweza kufikia siku ya leo. Mungu awakarimu sana na tuzidi kuombeana na kushirikishana fadhila. Karibuni soda tutakiane "Maisha Marefu"

Monday 22 October 2012

JUA KALI, HALI TATA ZA MAISHA



Kila kukicha hali ya maisha inaboreka kwa baadhi ya watu na inazidi kuwa tata kwa baadhi ya watu. Wakati wengine wanajitahidi kuboresha maisha, wengine mchana wa jua kali wanapata kinywaji asilia. Lakini tujiulize, mapumziko haya yanayosindikizwa na kinywaji hiki yanatokana na kwamba watu walishafanya kazi muda wa asubuhi, na hivyo wanastahili kupumzika au????

Sunday 21 October 2012

JUMAPILI NJEMA

Bado mapumziko ya wiki yanaendelea, nami niwatakie jumapili njema na mapumziko mema.

Saturday 20 October 2012

ADHA YA USAFIRI SI BONGO TU

Baada ya pilikapilika za siku nzima kuboresha maisha kwa kazi, jioni inapofika ni kipindi cha kurudi nyumbani kupumzika, lakini unapofikiria adha hii ya usafiri, uchovu unazidi. Lakini kwa wakati huo huo, kwa wenzetu hali tata ya usafiri inafanya magari kujaza sana na hata bodaboda ichukue zaidi ya abiria 7.


ASUBUHI HIVI....JIONI HIVI....


Maisha ni mzunguko. Leo mambo yapo hivi, kesho yapo vile. Japo ni mwisho wa wiki, nawasihi wadau wenzangu tuendelee kupambana kufanya maisha yaende mbele na kwa mafanikio maana mwisho wa siku nguvu zinakuwa zimepungua sana na utendaji kazi unapungu. Picha hizi zikufikirishe. Weekend njema wadau.

Friday 19 October 2012

KARIAKOO HALI SI SHWARI





Habari za hivi punde zinadai kuwa kuna hali mbaya katika maeneo ya Kariakoo jijini Dar e Salaam ambapo polisi wanapiga mabomu ya machozi kutawanya waislam wanaoandamana.
Kwa mujibu wa watu waliopo kwenye maeneo hayo maduka mengi yanafungwa na watu wanajifungia kwenye maduka hayo. Ingia hapa kwa taarifa zaidi:http://www.bongo5.com/breaking-kariakoo-pachafuka-mabomu-yanapigwa-kila-kona-10-2012/

KARIBUNI MLO WA MCHANA (LUNCH)

Wadau leo inabidi twende mpaka Bukoba ili lunch yetu inoge

NILIJUA UTACHEKA!


Jamaa watatu walikodi hoteli yenye gorofa 60, wao wakapata gorofa ya mwisho kabisa. Wakapanda kwa lifti na asubuhi wakashuka kwa lifti. Jioni waliporudi wakakuta umeme umekatika.
Wakakubaliana wapande ngazi kwa story. Wa kwanza akapiga story za kutisha kuanzia gorofa ya 1 mpaka ya 20, wapili akapiga strory za kuchekesha kuanzia gorofa ya 21-40 na watatu akandamiza story za kuhuzunisha kuanzia gorofa ya 41-60. Walipofika ya 59 yule watatu akasema hii ndio ya kuhuzunisha zaidi...TUMESAHAU KUCHUKUA FUNGUO PALE MAPOKEZI.

Hapa jamaa kaona kawin kweli kweli, kumbe hasara za kukumbia umande......soma kaka soma

ASUBUHI NJEMA

Labda tuanze siku yetu na kutafakari picha hii inayosisitiza kufungua macho. Watani wanasema, "kusoma hujui, hata picha nayo huioni"???

TUIGE LAKINI..........

Kwa sasa nchi yetu ya Tanzania ipo katika mchakato wa kupigia kura baadhi ya vivutio vilivyopo nchini(Serengeti, Ngorongoro, Mlima kilimanjaro, fukwe za zanzibar, mapango ya Amboni n.k.), ila walau kimojawapo kiingizwe katika orodha ya maajabu ya Dunia. Tuangalie na hiki kisijekuwa mojawapo ya maajabu.

Tuesday 16 October 2012

SHULE JAMANI SHULE

Hata baada ya miaka 50 ya Uhuru, nchi yetu inajitahidi kutengeneza maisha bora kwa kila mtanzania,. Hii ni pamoja na kuboresha elimu na mazingira yake, lakini kwa mtindo huu itwakuwaje???

HII NAYO KALI

Jeshi la Polisi nchini China
Polisi wa kike Marekani


Polisi nchi fulani Afrika

YA KWELI HAYO???

Ni kweli wa Moshi twapenda kutafuta hela, lakini tafsiri hii kiboko.