Thursday 30 June 2016

MHE WAZIRI MKUU AHAIRISHA VIKAO VYA BUNGE LA BAJETI

Waziri Mkuu mhe.Kassim Majaliwa akitoa hoja ya kuhairisha Kikao cha Bunge huko Dodoma leo.

USALAMA KUIMARISHWA VITUO VYA MABASI YAENDAYO KASI (DART)

Benjamin Sawe Maelezo

—————————–

Baadhi ya abiria wanaotumia usafiri wa mabasi yaendayo kasi maarufu kama mwendo kasi wameilalamikia kampuni hiyo kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya wizi vinavyoendelea katika baadhi ya vituo hivyo.

Bw. Juma Ally mkazi wa Kimara mwisho anasema vitendo hivyo hutokea nyakati za usiku kwa baadhi ya vijana kujifanya nao ni miongoni mwa watumiaji daraja hilo na kupelekea abiria kuibiwa vitu vyao ikiwa ni pamoja na kujeruhiwa.

Aliongezea kuwa walinzi wa kituo hicho wamekuwa wakifanya kazi ya kuwapanga abiria na kusahau majukumu yao ya kulinda usalama wa kituo hicho pamoja na mali zao.

“Tunashangaa hawa walinzi wanaolinda vituo hivi, abiria wamekuwa wakilalamika kila siku kuibiwa nyakati za usiku lakini tunaona abiria wakiendelea kuibiwa sijui wahusika wapo wapi?”Aliuliza Bw. Ally.

Nae Bi. Herrieth Shangaa aliongezea kuwa licha ya vitendo vya wizi vinavyoendelea katika vituo hivyo kuna baadhi ya vitendo vikiwemo vya kujisaidia katika madaraja hayo hivyo kupelekea uchafuzi wa mazingira

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msimamizi wa vituo hivyo ambae hakutaja kutajwa jina lake amesema kuna baadhi ya vituo ni vikubwa na wanawalinzi wachache hivyo wamejipanga kuongeza ulinzi ikiwa ni pamoja na kufunga mfumo wa kidigitali wa kudhibiti wahalifu

Mradi wa mabasi yaendayo haraka ulioanza rasmi terehe 10, mei, 2016 umeonesha ni jinsi gani kero ya foleni itakavyopungua kwa kuwa mabasi hayo yanatumia njia yake ambayo ni miundombinu iliyojengwa kwa gharama kubwa sana.

Wednesday 29 June 2016

TRAFIKI: HILO NDO LILILOWAPELEKA HUKO NJIANI

SHOGA ALIVYOTIKISA CLOUDS FM MAHOJIANO TAKE ONE

Shoga maarufu kwa jina la KAOGE

Mashoga wanaongezeka kwa kua waaribifu ni wengi na wengi ni watu wazito. Shoga anatamani kuzaa anataka kupandikiza na yupo kwenye harakati za kubeba mimba
Alikua anaitwa mwanamke tangu mdogo na baba yake na mitaani alikua anaitwa gody ka demu, Kiukweli wanaume tusifumbie macho ili swala malezi ya karibu zaidi tangu utoto ndio tunaweza kupiga vita USHOGA. Na si matusi kipigo na unyanyapaaji

Tuesday 28 June 2016

JELA MIAKA 30: KUMPA MIMBA,KUOA AU KUOLEWA NA MWANAFUNZI

BUNGE limepitisha kwa kauli moja Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya mwaka 2016 ambayo pamoja na mambo mengine, imeongeza adhabu kwa watu wanaowapa mimba au kuoa ama kuolewa na mwanafunzi, sasa watafungwa jela miaka 30.

Sheria hiyo ilipitishwa jana bungeni mjini Dodoma baada ya Muswada kuwasilishwa Juni 24, mwaka huu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ambao baadhi ya wabunge walipata fursa ya kuuchangia.

Muswada huo ulilenga kufanya marekebisho katika sheria 21 kwa lengo la kuondoa mapungufu yaliyobainika wakati wa utekelezaji wa sheria hizo na umepitishwa kuwa sheria.

Sheria zilizopendekezwa kurekebishwa na sheria hiyo ni pamoja na ya Kudhibiti Utakatishaji wa Fedha Haramu; Kudhibiti Usafirishaji Haramu wa Binadamu; Kanuni za Madai; Usajili wa Makandarasi; Elimu; Ajira na Mahusiano Kazini na Sheria ya Taasisi za Kazi.

Muswada huo uliowasilishwa bungeni na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju unatamka adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela katika marekebisho ya Sheria ya Elimu kwa watakaompa mimba, kumuoa au kuolewa mwanafunzi.

Awali adhabu iliyotamkwa katika sheria hiyo ya elimu ni mshitakiwa akibainika kuwa na kosa kutozwa faini ya Sh 500,000 na iwapo ni kosa la pili anatozwa faini ya Sh 500,000 au kifungo kisichozidi miaka mitatu.

Akiizungumzia sheria hiyo inayosubiriwa kusainiwa na Rais John Magufuli, Masaju alisema inawalinda watoto wote chini ya miaka 18 walioko na wasio shuleni na kuwa kosa hilo likifanywa na mtoto atahukumiwa kwa mujibu wa sheria ya mtoto.

Kifungu cha 60 A (i) kimeeleza kuwa itakuwa kinyume cha sheria katika mazingira yoyote yale kwa mtu yeyote kumuoa au kuolewa na mwanafunzi wa shule ya sekondari au ya msingi na atakayekiuka atafungwa jela miaka 30.

Katika Sheria ya Taasisi za Kazi inataka mwajiri anapokiuka masharti ya sheria ya kazi, ikiwa ni pamoja na kuchelewesha michango ya waajiriwa, kutoza faini na Ofisa wa Kazi ya papo kwa hapo isiyopungua Sh 100,000.

Wakichangia muswada huo, wabunge wameonesha furaha yao juu ya Sheria ya Elimu inayohusu adhabu ya miaka 30 jela. Hata hivyo, pamoja na furaha hiyo, baadhi ya wabunge wametoa angalizo la kutaka kupimwa kwanza DNA kabla ya kutoa hukumu huku wengine wakitaka kuwapo kwa nyongeza ya viboko.

Monday 27 June 2016

MHE WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MWIGULU NCHEMBAAKABIDHIWA OFISI NA MHE KITWANGA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto) akipokea taarifa ya makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo.

MHE RC MAKONDA AWAJIBU GAZETI NIPASHE

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda awajibu Gazeti la Nipase baada ya kumwandika Katika gaeti la Jana Jumapili June 27, 2016... 'Misifa ya Makonda kuwaponza wakongwe, wengi presha yapanda'... Ila yeye amendika maneno hayo juu, kwenye ukurasa wake wa Instagram

MHE RAIS MAGUFULI ATEUA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA PIA AFANYA MABADILIKO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.

Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.

Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.

Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali

Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
Arusha - Mrisho Mashaka Gambo
Arumeru - Alexander Pastory Mnyeti
Ngorongoro - Rashid Mfaume Taka
Longido - Daniel Geofrey Chongolo
Monduli - Idd Hassan Kimanta
Karatu - Therezia Jonathan Mahongo


DAR ES SALAAM
Kinondoni - Ally Hapi
Ilala - Sophia Mjema
Temeke - Felix Jackson Lyaviva
Kigamboni - Hashim Shaibu Mgandilwa
Ubungo - Hamphrey Polepole

DODOMA
Chamwino - Vumilia Justine Nyamoga
Dodoma - Christina Solomon Mndeme
Chemba - Simon Ezekiel Odunga
Kondoa - Sezeria Veneranda Makutta
Bahi - Elizabeth Simon
Mpwapwa - Jabir Mussa Shekimweli
Kongwa - John Ernest Palingo

GEITA
Bukombe - Josephat Maganga
Mbogwe - Matha John Mkupasi
Nyang'wale - Hamim Buzohera Gwiyama
Geita - Herman C. Kipufi
Chato - Shaaban Athuman Ntarambe

IRINGA
Mufindi - Jamhuri David William
Kilolo - Asia Juma Abdallah
Iringa - Richard Kasesela

KAGERA
Biharamulo - Saada Abraham Mallunde
Karagwe - Geofrey Muheluka Ayoub
Muleba - Richard Henry Ruyango
Kyerwa - Col. Shaban Ilangu Lissu
Bukoba - Deodatus Lucas Kinawilo
Ngara - Lt. Col. Michael M. Mtenjele
Missenyi - Lt. Col Denis F. Mwila

KATAVI
Mlele - Rachiel Stephano Kasanda
Mpanda - Lilian Charles Matinga
Tanganyika - Saleh Mbwana Mhando

KIGOMA
Kigoma - Samsoni Renard Anga
Kasulu - Col. Martin Elia Mkisi
Kakonko - Col. Hosea Malonda Ndagala
Uvinza - Mwanamvua Hoza Mlindoko
Buhigwe - Col. Elisha Marco Gagisti
Kibondo - Luis Peter Bura

KILIMANJARO
Siha - Onesmo Buswelu
Moshi - Kippi Warioba
Mwanga - Aaron Yeseya Mmbago
Rombo - Fatma Hassan Toufiq
Hai - Gelasius Byakanwa
Same - Rosemary Senyamule Sitaki

LINDI
Nachingwea - Rukia Akhibu Muwango
Ruangwa - Joseph Joseph Mkirikiti
Liwale - Sarah Vicent Chiwamba
Lindi - Shaibu Issa Ndemanga
Kilwa - Christopher Emil Ngubiagai


MANYARA
Babati - Raymond H. Mushi
Mbulu - Chelestion Simba M. Mofungu
Hanang' - Sara Msafiri Ally
Kiteto - Tumaini Benson Magessa
Simanjiro - Zephania Adriano Chaula

MARA
Rorya - Simon K. Chacha
Serengeti - Emile Yotham Ntakamulenga
Bunda - Lydia Simeon Bupilipili
Butiama - Anarose Nyamubi
Tarime - Glodious Benard Luoga
Musoma - Dkt. Vicent Anney Naano

MBEYA
Chunya - Rehema Manase Madusa
Kyela - Claudia Undalusyege Kitta
Mbeya - William Ntinika Paul
Rungwe - Chalya Julius Nyangidu
Mbarali - Reuben Ndiza Mfune

MOROGORO
Gairo - Siriel Shaid Mchembe
Kilombero - James Mugendi Ihunyo
Mvomero - Mohamed Mussa Utali
Morogoro - Regina Reginald Chonjo
Ulanga - Kassema Jacob Joseph
Kilosa - Adam Idd Mgoyi
Malinyi - Majula Mateko Kasika

MTWARA
Newala - Aziza Ally Mangosongo
Nanyumbu - Joakim Wangabo
Mtwara - Dkt. Khatibu Malimi Kazungu
Masasi - Seleman Mzee Seleman
Tandahimba - Sebastian M. Walyuba

MWANZA
Ilemela - Dkt. Leonald Moses Massale
Kwimba - Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
Sengerema - Emmanuel Enock Kipole
Nyamagana - Mary Tesha Onesmo
Magu - Hadija Rashid Nyembo
Ukerewe - Estomihn Fransis Chang'ah
Misungwi - Juma Sweda

NJOMBE
Njombe - Ruth Blasio Msafiri
Ludewa - Andrea Axwesso Tsere
Wanging'ombe - Ally Mohamed Kassige
Makete - Veronica Kessy

PWANI
Bagamoyo - Alhaji Majid Hemed Mwanga
Mkuranga - Filberto H. Sanga
Rufiji - Juma Abdallah Njwayo
Mafia - Shaibu Ahamed Nunduma
Kibaha - Asumpter Nsunju Mshama
Kisarawe - Happyness Seneda William
Kibiti - Gulamu Hussein Shaban Kifu

RUKWA
Sumbawanga - Dkt. Khalfan Boniface Haule
Nkasi - Said Mohamed Mtanda
Kalambo - Julieth Nkembanyi Binyura

RUVUMA
Namtumbo - Luckness Adrian Amlima
Mbinga - Cosmas Nyano Nshenye
Nyasa - Isabera Octava Chilumba
Tunduru - Juma Homela
Songea - Polet Kamando Mgema

SHINYANGA
Kishapu - Nyambonga Daudi Taraba
Kahama - Fadhili Nkulu
Shinyanga - Josephine Rabby Matiro

SIMIYU
Busega - Tano Seif Mwera
Maswa - Sefu Abdallah Shekalaghe
Bariadi - Festo Sheimu Kiswaga
Meatu - Joseph Elieza Chilongani
Itilima - Benson Salehe Kilangi

SINGIDA
Mkalama - Jackson Jonas Masako
Manyoni - Mwembe Idephonce Geofrey
Singida - Elias Choro John Tarimo
Ikungi - Fikiri Avias Said
Iramba - Emmanuel Jumanne Luhahula

SONGWE
Songwe - Samwel Jeremiah
Ileje - Joseph Modest Mkude
Mbozi - Ally Masoud Maswanya
Momba - Juma Said Irando


TABORA
Nzega - Geofrey William Ngudula
Kaliua - Busalama Abel Yeji
Igunga - Mwaipopo John Gabriel
Sikonge - Peres Boniphace Magiri
Tabora - Queen Mwashinga Mlozi
Urambo - Angelina John Kwingwa
Uyui - Gabriel Simon Mnyele

TANGA
Tanga - Thobias Mwilapwa
Muheza - Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
Mkinga - Yona Lucas Maki
Pangani - Zainab Abdallah Issa
Handeni - Godwin Crydon Gondwe
Korogwe - Robert Gabriel
Kilindi - Sauda Salum Mtondoo
Lushoto - Januari Sigareti Lugangika
Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Juni, 2016

Friday 24 June 2016

VIDEO: MHE RAIS MAGUFULI ASISITIZA USHIRIKIANO WA VYAMA

DK REGNALD MENGI ATOA MILIONI 70 KUCHANGIA MADAWATI

Mkurugenzi wa IIP Mdia Group Mhe.Dk Regnald Mengi ametoa mchango wa TZS Milioni 70 kusaidia ununuzi wa madawati katika shule za Wilaya ya Handeni na Bagamoyo

Thursday 23 June 2016

Wednesday 22 June 2016

KWA WANAOTAFUTA NYUMBA ZA KUPANGA

WABUNGE WA CCM NA UKAWA SASA KUCHUNIANA

Sakata la wabunge wa Ukawa kususa vikao vya Bunge vinavyoongozwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson limefika pabaya baada ya baadhi ya wawakilishi hao kuanza kutowasalimia baadhi ya wabunge wa CCM.

Hatua hiyo ilikuwa dhahiri jana baada ya Ukawa kutangaza kuwa hawatashirikiana na wabunge wenzao wa chama tawala katika shughuli za kawaida za kijamii, kama vile michezo na kutumia kantini ya Bunge, wakisema wenzao wameanza kuwabagua.

Mbali na kitendo hicho, wabunge hao pia walitoka kimyakimya bungeni baada ya Dk Tulia kuingia, lakini safari hii hawakufanya mbwembwe za kujiziba midomo kama walivyofanya juzi.

Jana asubuhi, mbunge wa CCM Kangi Lugola alisema kuwa alisikitishwa baada ya kudai kuwa Mbunge wa Chadema (Viti Maalumu), Lucy Magereli hakumjibu salamu yake wakati akiingia bungeni licha ya kumsalimia mara tatu na kuwa katika umbali mfupi wa kusikika.

“Kusalimia ni jambo la utamaduni wetu. Nilikuwa namsalimia mbunge wa kike wa Ukawa, lakini hakujibu. Lakini, nikajua ni sababu ya wao kufunga mdomo na plasta, nikamtania au kwa sababu ya plasta hujibu ili isije kudondoka hakuitikia,” alisema Lugola.

Alisema ameshtushwa na hali ilipofikia na hajui sababu za msingi za wabunge wa Ukawa kufanya vitendo hivyo, kinyume na udugu na utamaduni wa Watanzania.

Mbunge huyo machachari, alisema Kubenea alimziba mdomo Msigwa kwa mkono ili asizungumze chochote.

Naye mbunge wa Sumve (CCM ) Richard Ndassa alisema jambo wanalolifanya wabunge wa Ukawa siyo jema na halina tija kufanywa na wawakilishi hao wa wananchi.

“Sisi ni wabunge, hivi inapofikia kususa kuongea na wabunge wenzako, hatima yake nini?” alisema.

“Mimi nilienda kuwasalimia kama kawaida ambavyo huwa tunafanya kwa wabunge awe CUF, CCM au Chadema, sasa unavyosusa una maanisha nini,” alilalamika Ndassa.

Alisema kitendo cha kutosalimia ni cha juu sana na kwamba iwapo Ukawa wanashauriwa na mtu basi inawapasa kuchuja mambo mengine, likiwamo hilo la kuwasusa wabunge wenzao.

Juzi Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia wakati anawaongoza wabunge wa Ukawa kutoka bungeni aliwatuhumu wabunge wenzao wa CCM kuwa wanawabagua

Naye Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea alisema; “Leo tumekubaliana hatutashiriki katika michezo na wabunge wa CCM, hilo tumeanza leo asubuhi kwenye mazoezi katika viwanja mbalimbali, hivi sasa tunatafakari hata kutafuta uwanja wetu.

“Tukikutana katika uwanja mmoja, sisi tutatumia upande mmoja na wao watatumia upande mwingine, hatuchanganyani, hata salamu leo kuna mmoja kanisalimia nimekwepesha mkono wangu,”

Kubenea alisema hata katika mechi zinazoandaliwa kwa ajili ya timu ya wabunge UKAWA hawatashiriki katika kipindi hiki cha wiki mbili zilizobakia za bajeti.

“Si katika michezo tu, hata katika mahusiano, tumekubaliana kama kuna wabunge wana mahusiano ya kimapenzi na wabunge wa CCM yasitishwe kwa muda wa wiki mbili mpaka tutakavyoamua vinginevyo,” alisema Kubenea.

Tuesday 21 June 2016

TRUUMP ANUSURIKA KIFO

Mwanamume mmoja raia wa Uingereza Michael Sandford anayetuhumiwa kwa kupora bunduki ya afisa mmoja wa polisi katika mkutano wa kisaiasa wa Donald Trump, amewaambia wapelelezi wa Marekani kuwa, alitaka kumuua kwa kumpiga risasi na kumuuwa mgombea huyo wa kiti cha Urais wa chama cha Republican.
Kwa mjibu wa stakabadhi za mahakama, Michael Sandford anasema kuwa aliendesha gari hadi Las Vegas akiwa na nia ya kumpiga risasi Bw Trump siku ya Jumamosi.Awali Donald Trump alimtimua Maneja wake wa kampeni Corey Lewandowski kwa kutofautana naye katika kauli zake.

Monday 20 June 2016

BUNGENI DODOMA: WABUNGE UPINZANI WATOA KALI

Wabunge wa Vyama vya Upinzani vinavyounda Ukawa, leo wametoka tena Bungeni kama walivyoazimia kukacha vikao vyote vinavyoongozwa na Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson, lakini wamekuwa na mtindo wa aina yake.

Tofauti na siku nyingine, leo wabunge hao wa upinzani wamejifunika midomo kwa plasta huku wakiwa wameandika jumbe mbalimbali za kuonesha kuminywa kwa haki ya kujieleza.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia aliwaambia waandishi wahabari nje ya ukumbi wa Bunge hilo kuwa wameamua kutoka nje ikiwa leo ni siku ya kuipigia kura bajeti ya Serikali kwani hawakushiriki kuijadili. Pia, alisema kuwa bajeti hiyo ni mbaya inayowaumiza wananchi.

“Ni fedha za watanzania wote walipa kodi tukiwemo sisi. Lakini democratic perspective inasema ‘hakuna kulipa kodi kama hakuna uwakilishi’. Sasa sisi tunawaambia Watanzania, tumejadili na bajeti hii ni mbaya… mbaya sana ya kuwaumiza Watanzania. Ni ya maumivu mabaya sana ya kuwaumiza Watanzania,” alisema Mbatia.

Alisema kwakuwa leo ni siku ya kupiga kura hawatashiriki kwa kuwa hawakushiriki kujadili bajeti hiyo bali wataenda kushtaki kwa wananchi.

Akizungumzia zuio la mikuano ya hadhara, Mbatia amesema kuwa mikutano hiyo itafanyika tu kwani haipangiwi na mtu mmoja bali ni kwa mujibu wa sheria na taratibu za kidemokrasia.

Sunday 19 June 2016

HAPPY INTERNATIONAL FATHERS DAY

NAULI ZA MABASI YAENDAYO KASI SASA WAWEZA KUTUMIA PLASTIK CARD

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya MaxMalipo ambao wameingia ubia na Udart katika matumizi ya kadi hizo, Mhandisi Juma Rajabu (kulia), akizungumza katika mkutano huo. Kushoto ni Ofisa Habari UDART, Deus Bugaywa
Na Dotto Mwaibale

MRADI wa Mabasi Yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam (UDART) imeanzisha huduma kwa wateja wao za kutumia kadi maalumu wakati wa kupanda mabasi hayo itakayoanza rasmi leo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, Mkurugenzi Mtendaji wa UDART, David Mgwasa alisema wameanza kutoa huduma hiyo ya kadi ili kuwarahisishia wateja wao na kuondoa changamoto ya kusubiri tiketi kwa muda mrefu kabla ya kuondoka.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya MaxMalipo ambao wameingia ubia na Udart katika matumizi ya kadi hizo, Mhandisi Juma Rajabu alisema kwamba kwa kuanzia wametoa kadi 200,000 ambapo kila kadi itauzwa kwa shilingi 5000 ingawa bei halisi kwa kadi moja ni shilingi 500 na sh.4500 inayobaki itakuwa ni malipo ya mteja wao.

“Shilingi 4500 zitatumika kama malipo ya nauli kwa siku saba hadi nane kwa kwenda eneo lolote na kuwa kadi hizo zitapatikana katika vituo vya Kimara, Mbezi, Morocco, Gerezani, Posta na kuwa zitakuwa ni endelevu” alisema Rajabu

Aliongeza kuwa katika nchi nyingi zimekuwa zikitumia kadi hizo katika kusafirisha abiria na kuwa kwa hapa nchini ni huduma mpya ambayo itakuwa na changamoto zake kabla ya kuzoeleka.
Alisema licha ya kuanzisha huduma ya kadi bado ile ya risiti itaenelea kama kawaida ambapo alisema namna ya kujiunga na hu duma hiyo unatakiwa kupiga *152*22#

Saturday 18 June 2016

SAWA LAKINI HILI LINA DALILI ZA UCHOCHEZI

TUJIKUMBUSHE NOTI/FEDHA ZILIZOKUWA ZINATUMIKA TANZANIA MIAKA YA NYUMA

WADAU, HII IMEKAAJE KIMAADILI? UREMBO!!!!!

SAKATA LA ASKOFU GWAJIMA

BARUA YA WAZI KWA MHE FREEMAN MBOWE (CHADEMA/UKAWA)

Na Thadei Ole Mushi.

Kama ni mfuatiliaji wa siasa za Tanzania mbinu ya wapinzania kutoka njee ya bunge kwa sababu mbali mbali haikuanza leo. Na tangu wameaanza kuitumia mbinu hii haijawahi kuwasaidia au hata kueleweka kwa wananchi badala yake sisi wananchi ndio huwa tunapata hasara.

Kwa mara ya Kwanza wapinzani walitoka njee ya Bunge wakati raisi Kikwete alipoingia madarakani kwa mara ya pili kwa kile walichokidai kuwa ni kutomtambua. Walitoka njee wakati wa kuhutubia bunge na kulifungua bunge.

Je waliposusia bunge mwisho wa siku hawakuja kumtambua raisi Kikwete?? jibu ni NDIO wakikuja kumtambua na walivunja rekodi kupiga hodi ikulu kuomba busara za raisi kuliko vipindi vingine vyote.Tuliwashuhudia wakiburudika na juice mara nyingi tu Ikulu wakipata picha ya pamoja nk.

Mara ya pili tunawaona upinzani ukitoka njee kususia bunge la katiba. Mwisho wa siku bunge liliendelea na katiba pendekezwa ikapitishwa bila kuwa na mawazo mbadala ya wapinzani ndani ya katiba ile inayosubiria kupigiwa kura.

Mara ya tatu upinzani unatoka njee kupinga matokeo ya uraisi yaliyompa raisi Magufuli ushindi. Wanatoka siku ya raisi kulifungua bunge kama walivyotoka kipindi cha Kikwete. Raisi analifungua bunge na baada ya hapo bunge lilelile lililopewa uhalali na rais Magufuli baada ya kulifungua wapinzani wanarudi na kulitumia. Na hata sasa wapinzani wameshamtambua raisi Magufuli kuwa ni raisi halali na aliyechaguliwa kihalali.

Mara ya nne ni hili la kumkimbia Dr Tulia. Katika hali ya kawaida nilifikiri wangelifanya hivi kwa siku moja tu. Mpango wa kususia kila siku kumetuathiri sana sisi wananchi kuliko kulivyomuathiri Dr Tulia. Tena wapinzani wanatoka njee kipindi muhimu kabisa ambacho walipaswa kuombea majimbo yao miradi ya kimaendeleo toka kwenye bajeti ambayo itapitishwa muda mfupi ujao.

Upinzani umetoka kwenye mstari wa kujenga hoja hadi kususia kususia mambo ya ajabu ajabu.Nakiri kabisa kuwa kilichoijenga kambi ya upinzani nchini ni hoja zao nzito miaka ya 2005-2015.

Sote tunakumbuka jinsi upinzani ulivyopata umaarufu kwa kujenga hoja za kukataa ufisadi, kudai katiba mpya, swala la Buzwagi, na hata juzi juzi swala la ESCROW. Kafulila pamoja na kutukanwa tumbili alisisimama kidete hadi akafanikiwa kuwangoa kina Warema bungeni na wengineo. Nataka nikuonyeshe nguvu ya hoja ilivyo na mantiki kuliko hii zomea zomea na kutoka nje ya bunge.

Katika nchi zote za jumuiya ya Madola Tanzania upinzani ndio unaongoza kwa kuthaminiwa kuliko nchi zote. Thamani hii upinzani umeshindwa kuutambua na kuutumia kujijenga badala yake wamekimbia na kinachowakimbiza ni kanuni walizojiwekea wenyewe.

Ni Tanzania tu katika ukanda huu Kambi rasmi ya upinzani inatambulika bungeni, kuwa na baraza la mawaziri kivuli, na baadhi ya kamati nyeti zinazogusa maslahi ya Taifa kuwekewa kanuni lazma ziongozwe na upinzani kama PAC nk.

Hii ni fursa ambayo upinzani walipaswa kuitumia kujitangaza kuliko kuzurura njee ya viwanja vya bunge. Inauma sana kuona wanakosea na hawataki kujirekebisha.

Naamini si wabunge wote wa upinzani wanataka kutoka njee ya Bunge lah hasha. Prof Elton Mayo aliwahi kutoa nadharia ya Hawthorne Effect, nadharia ya kisaikolojia ambapo mtu hufanya jambo kwa kuwa tu kuna mtu anayemsimamia kufanya hivyo au anafanya tu kwa kuwa anajua anaonekana anachokifanya. Hivyo unafanya jambo si kwa kuwa unapenda kulifanya ila unafanya kwa kuwa kuna sababu zinakufanya ufanye.Nikiangalia huu utoto anaoufanya Mbatia pamoja na uelewa wake wote naona madhara ya mob psychology.

MBOWE nakuomba usitumie tena mbinu hii haiwajengi inawabomoa.

Ole Mushi.

MwanaCCM mwenye kujali maslah mapana ya nchi.

Friday 17 June 2016

MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO

Wakati tukijionea matukio mbalimbali ya utovu wa nidhamu,umaskini na uvunjifu wa amani katika jamii,ni dhahiri msemo huu wajidhihirisha. Mtoto akilelewa vizuri,hukua vizuri katika nyanja zote za maisha. Lakini asipolelewa vizuri ni chanzo cha vurugu katika jamii

KATUNI YA LEO NA MCHAKATO WA KUZIMA SIMU FEKI

Wednesday 15 June 2016

MHE RAIS MAGUFULI AFUTARISHA

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea machache baada ya futari ya pamoja ya viongozi mbalimbali wa dini aliyoandaa Ikulu jijini Dar es salaam Jumanne Juni 14, 2016
(Chini)....Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika foleni na wageni wake kwenda kuchukua chakula wakati wa kufuturu katika futari ya pamoja ya viongozi mbalimbali wa dini aliyoandaa Ikulu jijini Dar es salaam Jumanne Juni 14, 2016

ANGALISHO: SIMU FEKI ZINAZIMWA KESHO 16 JUNI 2016

Tuesday 14 June 2016

VIDEO: SIKILIZA MANENO YA HEKIMA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA

MHE PROFESA LIPUMBA BADO HAKIJAELEWEKA KUHUSU KURUDI CUF

Wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akitengua uamuzi wake wa kung’atuka kwenye wadhifa huo na kuomba kurejea, viongozi wa juu wa chama hicho wamepinga hatua hiyo wakisema katiba yao hairuhusu na kwamba anakwenda kukiua chama.

Kauli za viongozi hao, zimekuja muda mfupi baada ya Profesa Lipumba kutangaza nia hiyo jana kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho, Buguruni huku akibainisha kuwa amefanya hivyo baada ya kuombwa.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema Lipumba hawezi kuwa na nia njema ya kukijenga chama hicho endapo atarudishwa kwenye nafasi aliyoikataa.

“Anataka kuja kukiharibu chama,” alisema Mazrui. Alifafanua kuwa tayari chama hicho kimefanya mambo mengi bila Lipumba ambaye alikuwa anaona kila kinachoendelea, hivyo alichokisema hakina mashiko kwani CUF ilisharidhia kuitisha mkutano wa uchaguzi kujaza hiyo.

Akieleza sababu alizozitoa mwenyekiti huyo, Mazrui alisema haoni chochote cha maana. “Sababu zilizomuondoa zingalipo. Kinachomrudisha ni nini?” alihoji naibu katibu mkuu huyo.

THIBITISHA KAMA SIMU YAKO NI ORIGINAL AU FEKI KABLA YA KUZIMWA 16 JUNE

Monday 13 June 2016

PROFESA LIPUMBA ATENGUA UAMUZI NA KUAMUA KUOMBA KURUDI KATIKA NAFASI YAKE CUF

HATIMAYE Prof. Ibrahim Lipumba, aliyekuwa Mwenyekti wa Chama cha Wananchi (CUF) ametangaza kurejea kwenye nafasi yake ya uenyekiti-taifa wa chama hicho.

Amesema, anarejea kwenye nafasi hiyo baada ya muda wa kutosha alioutumia kutafakari siasa za nchini na namna demokrasia inavyokanyagwa na watawala wa nchi hii.

“Nimemwandikia Katibu Mkuu (Maalim Seif Sharif Hamad) kutengua barua yangu niliyoandika 5 Agosti mwaka jana,” amesema Prof. Lipumba.

Prof. Lipumba alijiuzulu nafasi yake mwaka jana kwa madai ya kutoridhishwa na uamuzi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kumridhia Edward Lowassa kupeperusha bendera ya umoja huo kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 kupitia Chadema.

Hata hivyo amesema, analazimika kurejea kwenye nafasi ya uenyekiti wa chama hicho taifa kutokana na kuguswa na matatizo ya demokrasia nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam amesema kuwa, amemuandikia barua Maalim Seif ili atengue uamuzi wake wa awali wa kuachia nafasi hiyo.

Katiba ya mwaka 1992 Toleo 2013 Ibara ya 117 inaeleza kwamba, barua ya kujiuzulu inapaswa kujadiliwa na Mkutano Mkuu kujadili jambo ambalo mpaka sasa halijafanyika.

Prof. Lipumba aliteuliwa kutwaa nafasi hiyo na Mkutano Mkuu mwaka 1999. Ibara hiyo inaipa mamlaka mkutano huo kukubali ama kukataa kujiuzulu kwake na kwamba, kauli yake ya leo kuwa Maalim Seif atengue barua yake inatokana na kutokwenda kwenye ngazi hiyo (Mkutano Mkuu) nyingine ya uamuzi.

Prof. Lipumba amesema kuwa, dhuluma iliyofanyika katika visiwa vya Zanzibar ya kuporwa kwa haki ya wananchi, imemsukuma kurejea kwenye mapambano ya haki nchini.

Amesema, demokrasia ya Tanzania ina matatizo akitaja miongoni mwayo ni Bunge kuendesha kwa itikadi ya chama.

Pia amesema kuwa, uongozi wa Rais John Magufuli unaonekana kuwa wa kasi isiyojali Demokrasia.

Akizungumzia Zanzibar amesema, chama chao na watanzania wapenda haki hawatambui utawala wa Dk. Ali Mohammed Shein visiwani humo kwa kuwa hakupatikana kwa njia halali ya kidemokrasia.

Amesema kuwa, Rais Magufuli asipozingatia misingi ya demokrasia nchi haitakuwa na uwajibikaji

WAHESHIMIWA MWIGULU NCHEMA NA CHARLES TIZEBA WAAPISHWA KUWA MAWAZIRI

Thursday 9 June 2016

MCHEZAJI WA NBA HASHIM THABEET AFANYA MAONGEZI NA MAKAMU WA RAIS MHE SAMIA SULUHU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mchezaji wa kikapu wa kulipwa nchini
Marekani, Mtanzania Hashim Thabeet, wakati alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar
es salaam leo Juni 09,2016 kwa ajili ya kumuelezea kuhusu lengo na mpango wake
wa kuanzisha na kukuza michezo pamoja na vituo vya Michezo
hapa Nchini.

DODOSA YA MAGAZETI KUHUSU BAJETI YA 2016/2017

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Philip Mipango akiwa amenyanyua Mkoba ulokuwa na makabrasha ya Bajeti