Sunday 3 January 2016

KATUNI YA LEO

Masoud Kipanya tena, anawasilisha tatizo lililopo katika wakati uliopo. Ni sahihi, si kila jambo ni la kumsubiri Magufuli. Ni wajibu wa jamii. Na mwalimu huyu naye ni sehemu ya jamii. Je, ni sababu zipi zinazompelekea aache kufundisha na kufanya biashara ya bodaboda? Kama kazi ya ualimu aliomba mwenyewe, hakulazimishwa. Na kama mshahara anapata kwa wakati. Hana sababu ya kufanya anachofanya wakati wa kazi, labda iwe jioni au kwenye likizo yake. Na hata kama ni jioni na kwenye likizo, mwalimu hapaswi kuonyesha mfano mbaya kwa kubeba abiria mishikaki!

No comments:

Post a Comment

Maoni yako