Wednesday 20 January 2016

BODABODA: HII SASA MMEPITILIZA

Linapokuja suala la usafiri wa haraka na uhakika,bodaboda zimekuwa na mchango mkubwa sana, ila kwasasa ukiukwaji wa sheria hasa usalama limekuwa kubwa. Ni muhimu kuzingatia usalama wa abiria kwa vigezo vilivyoweka mfano kuvaa Helmet, kupatia abiria mmoja tu kwa wakati mmoja, mwendo kasi....
KATIKA kukabiliana na madereva wa pikipiki wanaopakia abiria zaidi ya mmoja maarufu mshikaki, Jeshi la Polisi mkoani Pwani litatumia mbinu mpya ya kuwapiga picha madereva hao na kuwakamata baadaye wakiwa kwenye vituo vyao.

Jeshi hilo litatumia mbinu hiyo ili kuepusha ukamataji kwa kuwakimbiza wale wanaofanya hivyo kwa lengo la kuepuka kusababisha ajali wakati wa kuwakamata madereva hao wanaobeba mshikaki.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako