Friday 31 October 2014

KATUNI YA LEO

Tazama namna ushirikina unavyoleta ukatili dhidi ya ubinadamu.

Thursday 30 October 2014

TUCHAPE KAZI ILA KWA UMAKINI

Chombo hiki kinachosaidia kuingiza kipato hakika hakitumiki vizuri. Kama kweli wahitaji kipato endelevu, jali na tunza pia kifaa cha kazi.

SIMANZI ZAMBIA

Ni juzi tu wamesherehekea miaka 50 ya Uhuru wa nchi yao, ila jana Zambia imempoteza Rais wao Mhe. Sata huko London alipokuwa akipata matibabu. Habari zinasema Makamu wa Rais Mhe. Dk, Guy Scottambaye ni wa asili ya Kizungu ndio anashika madaraka mpaka uchaguzi utakapofanyika tena. RIP Rais wa Zambia.
Mhe. Dk. Guy Scott

UTANI MWINGINE WAHITAJI UJASIRI

Watoto wana namna nyingi za kufanya matani ila matani mengine yahitaji ujasiri mkubwa kuyakubali . Hapa huyu mtoto akiamua kufanya majaribio ya matumizi ya hilo panga, anafungua bucha. Tuwafundishe watoto wetu matani mazuri na yafaayo katika kujijenga binafsi na jamii. Ila pia tuwakumbushe matani mengine ambayo yanaweza kuleta madhara.

HUU NAO NI UBUNIFU

UBUNIFU

Katika kuboresha maisha na kuleta mvuto zaidi kimazingira, ubunifu ni muhimu.
Ubunifu katika michezo

Tuesday 28 October 2014

MISAADA ISIVYOTUMIKA VIZURI

Hivi kweli tuliomba msaada wa net kujikinga na malaria au kuzikinga mboga zetu na malaria au wanyama/ndefu/wadudu waharibifu?

YAWEZEKANA KWELI KWAMBA MADREVA WETU HAWAJUI KUSOMA AU NI DHARAU???

Monday 27 October 2014

KUMEKUCHA TUKAWAJIBIKE

Tulikotoka ni mbali , pengine asubuhi hii ndo unapasha ugali moto ule uwahi majukumu yako kama ni shule au kazini. Yote maisha, twende tukawajibike.
Tukauze mitumba sasa Gulioni
Nawe Boda boda usijali, hii ni zaidi ya Mshkaki
Mavuno ya mshambani nayo

Sunday 26 October 2014

NAWATAKIA JUMAPILI NJEMA

USALAMA BARABARANI "F"

URAIS NI WITO

UHUSIANO KATI YA TANZANIA NA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

Mhe.Rais Jakaya Kikwete akiangalia mchoro wa ramani ya Tanzania unayoonyesha Reli ya Kati inayotarajiwa kufanyiwa ukarabati mpya na wa kisasa na Kampuni ya China, alipokuwa ziarani China wiki hii. Ukarabati huo utahusisha Reli ya kati ya Dar es Salaam-Kigoma, Tabora-Mwanza, Kaliua-Mpanda-Ziwa Tanganyika
Mhe.Rais Kikwete akisalimiana na mwenyeji wake Rais wa China mhe. Xi Jinping

Monday 20 October 2014

KATUNI ZA LEO

Kwa hisani ya Global Publishers

MAPENZI YA MUNGU: FILAMU YA LULU NA MAMA KANUMBA

Mwezi, Wiki na Sasa siku zimebaki kwa ile Filamu Mpya na ya Kusisimua ya MAPENZI YA MUNGU Kuingia Sokoni ambayo imewakutanisha wasanii mahiri wa hapa hapa Tanzania ambapo Mmoja kati ya Wasanii waliocheza filamu hiyo Ni Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya anayejulikana kama Linah Sanga, kwa Kushirikiana na Elizabeth Michael LULU bila Kumsahau Flora Mtegoha ambae ni Mama Mzazi wa Marehemu Steven Kanumba watakuwa ndani ya filamu Mpya iitwayo MAPENZI YA MUNGU...Ni Filamu ambayo Kisa chake
na Mafunzo yake yanasisimua lakini Pia ni Moja kati ya filamu ambayo kiukweli ina hadhi na vigezo vya kimataifa...... Nimefika hapa leo sio kwa Ujanja wangu Bali ni Kwa "Mapenzi ya Mungu..."
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" ni moja ya filamu ambayo Msanii Linah pamoja na Mama Mzazi wa Marehemu Kanumba wameonyesha uwezo wa hali ya juu na kuthibitisha kuwa kweli Sanaa ni Kazi.
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa Sokoni Kuanzi Wiki hii Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.
Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd.

YASEMAVYO MAGAZETI LEO

MAAJABU YA MTI TABORA

Pichani ni mti unaodaiwa kunyanyuka ghafla baada ya kuanguka miaka mitatu iliyopitakatika kijiji cha Mfuto kata ya Ufuluma ,ambapo wilaya ya Uyui mkoani Tabora.
Katika hali ya kushangaza huku kila mtu akifikiria yake baaya ya juzi huko mkoani Tabora, kutokea tukio la aina yake ambapo inaelezwa kuwa mti aina ya Msufi uliokuwa umeanguka yapata miaka mitatu iliyopita umesimama ghafla tena kwa sauti kubwa ya mrindimo na kuwafanya wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo.

EBOLA YALETA HOFU MWANZA

Watu sita wakiwamo wahudumu watatu wa afya wa hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza, wamewekwa chini ya uangalizi maalum baada ya kumhudumia mgonjwa aliyefariki akiwa na dalili za ugonjwa wa ebola.Mtu aliyefariki alitajwa kuwa ni Salome Richard (17), anayetoka katika kijiji cha Kahunda wilayani Sengerema.

Akithibitisha kuwapo kwa hali hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitali Teule ya Wilaya ya Sengerema, Dk. Mary Jose, alisema mgonjwa huyo alifikishwa katika hospitali hiyo na ndugu zake watatu akiwa na homa kali huku akitokwa na damu sehemu mbalimbali za mwili wake.Alisema vipimo vya mgonjwa huyo vimepelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Nairobi Kenya kwa uchunguzi zaidi.

Sunday 19 October 2014

MAPUMZIKO YA MWISHO WA WIKI YAMEISHA

Wengine wanavyowaza, weekend inapokaribia kuisha.....

Saturday 18 October 2014

TULIOKATAA VIJIJI VYA UJAMAA,MNASEMAJE HAPA

Nyumba 38 zilizojengwa karibu kabisa na makao makuu ya wilaya ya Uyui huko Isikzya Tabora.Ni katika mpango mzima wa mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu.

HII IMEKAAJE???

CCM KUNANI??????

WHEN IN ROME,DO AS ROMANS DO" UKIWA ROMA ISHI KAMA WAROMA WANAVYOISHI

Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe.Anna Makinda akiwa Muscat kwa ziara rasmi za Kibunge
Mhe.Spika akiwa na ujumbe wake alipokutana na wenyeji wake huko Muskat. Shela/hijab inahusu!

Friday 17 October 2014

WAMEPENDEZAJE?

Ni ijumaa, wiki ya masomo imeisha kwa shule za msingi. Basi wao wanarudi nyumbani wakiwa wametokelezea kivyao. Hapana chezea fashion wewe.

BUSARA YA LEO: MAMBO YA KUJITAHIDI KUFANYA KABLA YA KUFIKIA MIAKA 30

1. Tambua uwepo wa Mungu na jitahidi kuzingatia maadili ya imani yako.
2. Jifunze kuweka akiba ya fedha tena bila kuigusa aidha benki au taasisi za fedha
3. Tafuta mpenzi sahihi na tulia nae kupanga maisha
4. Ishi mahali pa peke yako, sio kukaa na washkaji au mashoga tu
5. Lipa madeni yako ya zamani yote. Pia watake radhi mliokosana, jenga amani na watu.
6. Jenga mwili wako na jitahidi kutunza afya yako.
7. Jitahidi kuwa na marafiki wanaokujenga na kukupa changamoto za kimaendeleo za maisha.
8. Anza kuweka vitega uchumi kama kununua ardhi, biashara n.k
9. Jitahidi kuvaa kwa heshima sio ili mradi tu. Kata K na vimini sio dili
10.Tambua na ukubali kuwa umekua na uache tabia za kitoto au kufuata mkumbo.
11.Yaache ya zamani yapite na uanze upya.

Thursday 16 October 2014

CCM NA WOSIA WA BABA

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa CCM kwenye ukumbi wa NEC,CCM Makao Makuu Dodoma.

MELI KUBWA KULIKO ZOTE DUNIANI KWA SASA

Meli ya Oasis Seas ndio inayoongoza kwa ukubwa. Ina uwezo wa kuchukua abiria 6,300 na wahudumu 2394 kutoka zaidi ya nchi 71. Ndani ina kila aina ya maraha. Imetia nanga katika Bandari ya Southampton huko Uingereza.
Ramani ya meli hiyo

Wednesday 15 October 2014

UTAALAMU WA HALI YA JUU WA TANESCO NA TANROAD

Nguzo hii ya Umeme ipo barabarani maeneo fulani huko Mbeya. Sasa sijui wahusika ndo wameona hapo ndo utaalamu wao wote umetumika hadi kufanya hivyo au hawaona kama kuna tatizo

NGUO ZA JESHI WAACHIE WANAJESHI

Raia huyu alikutwa na adha hiyo maeneo ya Kariakoo baada ya kukutwa amevaa majazi ya jeshi ilihali yeye si mwanajeshi

KIONGOZI: MTU WA WATU

MAGAZETINI

SHULE ZETU,ELIMU YETU,WALIMU WETU NA WANAFUNZI WETU???

Tuesday 14 October 2014

NYERERE DAY

WATANZANIA leo tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 15 tangu kufariki kwa muasisi na Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwalimu Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999 akiwa nchini Uingereza alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa ya damu.
Maadhimisho ya siku hii kitaifa yamefanyika huko Tabora sambamba na sherehe za kuzima Mwenge mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe Jakaya Mrisho Kikwete
Juu ni picha wakati wa siku za maombolezo ya kifo cha Baba wa Taifa mwaka 1999
Kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka huu ndg Rachel Kassandra akimkabishi mhe,Rais Kikwete mwenge wakati wa kilele cha mbio hizo huko Tabora
Makamanda wa Mwenge wa Uhuru