Monday 25 January 2016

ANGALISHO: BONGO MOVIES 'MNAIGIZA HADI KUIGIZA'

Nimekuwa nikijiuliza kwanini Tasnia yetu ya Bongo Movies inaonekana kusua sua katika soko la ndani na hata Kimataifa? maana ukiangalia movies tunazoangalia watanzania wengi ndani na nje ya nchi sio za nyumbani bali za mataifa mengine na kwa Afrika ni Movies za Nigeria (Nollywood). tatizo ni nini? Jibu ni rahisi sana; Bongo Movies ubunifu na umakini katika tasnia unasua sua.

ANGALIA PICHA HII HAPA CHINI........................

Huyu ni Jambazi mwenye silaha anamvamia mwanadada nyumbani kwake ili kumpora, lakini angalia miguuni kavua viatu asichafue tiles. Huo muda wa kutoka nje na kuvaa viatu atapata wapi??? Mwingine unakuta mfano ni mwanadada anamwekea mume wake sumu kwenye juice afu akishakoroga anaonja kama imekolea, inawezekanaje? Kwa haya na mengine mengi mtamshawishi vipi mtanzania apende kazi zenu?

No comments:

Post a Comment

Maoni yako