Saturday 31 October 2015

MJUE "FIRST LADY" WA TANZANIA 2015-2020

Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli akimtambulisha mke wake Janeth Magufuli mbele ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliokuja kumpongeza

ZANZIBAR HALI TETE

WAKATI HUO HUO,....................

Jeshi la Polisi Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi (JWTZ), limefanikiwa kuteguwa bomu lilitegwa eneo la Mkunazini karibu na kituo cha polisi mjini Zanzibar.
Bomu hilo lilitegwa na watu wasiofahamika na jeshi la polisi lilipata taarifa ya kutegwa kwa bomu hilo kutoka kwa wasamaria wema.

MHE.DK. MAGUFULI AANZA KUMWAGA CHECHE BAADA YA KUKABIDHIWA HATI YA USHINDI


Rais Mteule Dk John Magufuli ameamua kufunguka kuhusu ugumu aliokabiliana nao wakati wa mchakato wa kampeni akieleza kuwa uchaguzi wa mwaka huu umekuwa na changamoto kubwa kutokana na hujuma zilizofanywa na wanafiki waliojificha ndani ya Chama cha Mapinduzi(CCM).

Amesema amekerwa na hali hiyo kiasi cha kushindwa kuvumilia kuizungumzia jana, hasa baada ya kuona uchaguzi umekwisha, hivyo ni vyema wanafiki hao wakajisalimisha kwa kutubu kwa kuwa wamekigharimu chama hicho na kusababisha kiwe kwenye wakati mgumu.

Amesema kwamba asiposema atakuwa ni mnafiki kwa sababu uchaguzi umekwisha bora wawekwe wazi kwa sababu anaona ni bora kuishi na mchawi kuliko mnafiki, alimuomba Mwenyekiti wa chama hicho Jakaya asiwahurumie wanaokihujumu, hivyo kusababisha washindwe kufika kwenye malengo.

“Nisiposema nitakuwa mnafiki msema kweli ni mpenzi wa Mungu watubu wajirekebishe ni mara kumi kuwa na mpinzani kutoka nje kuliko ndani ya chama,mipango yenu mtaipanga mchana usiku wataitoa nje ni afadhali uwe na mchawi atakuroga ufe kuliko mnafiki ndani, ” amesema Maguli katika hafla ndongo ya kumpongeza baada ya kukabidhiwa cheti na kuongeza:

“ Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli wewe ni mwenyekiti lakini ulikaa na wanafiki ndani ya CCM, ndiyo wametufanya wakati mwingine tufike hapa tulipofika, ndiyo wametufanya tufike hapa tulipo , leo kwa hiyo nakuomba ukitengeneze chama chetu vizuri ukishamgundua mnafiki usikae naye fukuza kesho, nimeona hili nilizungumze lakini unisamehe sana kwa sababu ningebaki nalo moyoni ningenisababishia kiungulia,ambacho nimekiona wakati nazunguka nikiwa kwenye kampeni,”


Kuanza kazi haraka
Magufuli amewahakikishia wananchi kuwa mara baada ya kuapishwa siku hiyo hiyo atanza kufanya kazi, kwa kuwa hakuomba nafasi hiyo kwa majaribio bali kuwatumikia wananchi kwa dhati.

Pia ameomba ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi ili waweze kufanikisha yale ambayo wameahidi wakati wa kampeni yeye na na Makamu Rais Samia Suluhu Hassan, ili waweze kutimiza wajibu wa kuwatumikia bila kinyongo na kuyatimiza yake waliyoahidi wakati wa kampeni.

“Kwa hiyo niwaombe ndugu zangu watanzania wote bila kujali vyama vyetu tunaomba sana ushirikiano wenu , tusipopata ushirikiano wetu hatuwezi kuyatimiza kwa wakati, tisipopata ushirikiano mzuri kutoka kwenye mtatuchelewesha mara unataka kufanya hizi mara kuna maandamano yakashindwe, yakalegee yakabaki huko huko yalikoanzia, kwa sababu sisi tunataka tufanye kazi,” alisema Dk Magufuli na kushangiliwa.

Aliongeza kusema“ Katika kuzunguka kwetu kwa wananchi wameona kuna kero nyingi za maji, umeme, miundombinu, wananchi wanataka zitatuliwe haraka, niwaombe watanzania bila kujali vyama naomba ushirikiano wenu mzurI, ili tufanikishe hayo tuliyoahidi wakati wa kampeni,” alisisitiza.

Amsifu JK
Rais huyo Mteule alimsifu Rais wa awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete akisema kwamba ni wa tofauti kwani licha ya kumtembeza katika maeneo karibu yote ya Ikulu , lakini pia amekuwa na busara za kukubali na kuendeleza madaraka ya kupokezana.

“ Nataka niseme mheshimiwa Rais una moyo wa pekee, Mungu akujalie sana viongozi wengi Afrika wanapokaribia kuondoka madarakani wengine huwa wanatengeneza hata katiba tofauti ili katiba ili waendelee kubaki madarakani, lakini wewe upo tayari kuondoka hata leo,” alisema.

Dk Magufuli alisema anaamini kwamba wananchi wataendelea kumuombea, kumlinda kwa kuwa amethamini Tanzania Kwanza, hivyo ataendelea kuhitaji busara zake pale itakapobidi atakapoingia madarakani.

Awali akitoa maoni yake mara baada ya Dk Magufuli kukabidhiwa cheti cha ushindi, Mratibu wa Taifa wa ULINGO, Dk Ave Maria Semakafu alisema anaamini wanawake wengi wamefurahishwa na ushindi huo kwa sababu kwa umewezesha pia kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi kuwa na Makamu wa Rais mwanamke Samia Suluhu Hassan.

“ Tumefungua ukurasa mpya kwani miaka 20 ya tamko la Mkutano wa wanawake Duniani wa mwaka 1995 Beijing, tumekuwa na mrejesho mzuri kuhusu mwitikio wa Serikali kuweka ushiriki sawa wa nafasi za uongozi badala ya kuwafanya wanawake wawe watu wa kupiga kura kwa kuchagua viongozi wa ngazi mbalimbali lakini sasa nao wanachaguliwa, wanaaminika na kupewa nafasi kubwa ya uongozi kama hii,”
alisema Dk Semakafu .

Alisema uchaguzi wa mwaka huu umekuwa ni wa kihistoria katika mambo mengi licha ya ushindani wa kisiasa lakini wanawake wawili walikuwa ni wagombea akiwamo Anna Mgwira aliyekuwa akigombea nafasi ya urais kupitia chama cha ACT Wazalendo.

“ Binafsi nilikuwa nafuatilia kwa karibu kampeni zao kulikuwa na mwitikio mkubwa wa watu walikuwa wakiwasikiliza na hakukuwa na hali ya udhalilishaji wa kuona kwamba hawastahili kwa sababu tu wao ni wanawake ,” alisema .

Friday 30 October 2015

VIDEO: MWL NYERERE ALIPOONYESHA WASIWASI WAKE KHS KUWAKABIDHI NCHI WAPINZANI

VIDEO: RAIS MTEULE AKABIDHIWA CHETI CHA USHINDI

UZALENDO WA KWELI

Mshindi wa kinyang’anyiro cha Urais kwa tiketi ya CCM na Rais Mteule Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipokea salamu za pongezi kutoka kwa mgombea Urais Mwanamke Pekee kwa tiketi ya ACT Wazlendo Mama Anna Mghwira mara baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva kutangaza rasmi matokeo ya uchaguzi mkuu Ikulu jijini Dar es salaam ambako yeye na Rais Jakaya Mrisho Kikwete walifuatilia kwa pamoja matangazo hayo ya moja kwa moja kupitia vituo vya televisheni. Dkt Magufuli amemshukuru sana Mama Mghwira na kumwita mkomavu wa siasa na mwana-Demokrasia wa mfano jioni hii Oktoba 29, 2015

MAGUFULI: ALIKOTOKA NI MBALI

MAGUFULI MAGAZETINI

BAADA YA MATOKEO YA URAIS KUTANGAZWA, SAFARI YA KWENDA.......IMEANZA

Hii ni kama alivyojitabiria yeye mwenyewe

HONGERA RAIS MTEULE DKT.JOHN MAGUFULI

Tume ya uchaguzi ya Tanzania Bara (NEC) kupitia Mwenyekiti wake Jaji Damian Lubuva imemtangaza Rasmi mgombea Urais wa CCM, Dr John Pombe Magufuli kuwa mshindi halali wa kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya jumapili wiki iliyopita.

Kwa Mujibu wa jaji Lubuva, Dr magufuli amepata ushindi wa kura Milioni 8 ( 8,882,935 ) sawa na asilimia 58.45% huku akimwacha kwa mbali mpinzani wake wa karibu , Edward Lowassa (Chadema ) ambaye amepata jumla ya kura Milioni 6 ( 6,077,848 ) sawa na asilimia 39.97%

Dkt. Magufuli na mgombea mwenza, Samia Suluhu watakabidhiwa rasmi vyeti vya ushindi tar 30 Okt saa nne asubuhi katika ukumbi wa hoteli ya Diamond Jubilee
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza kwa furaha mshindi wa kinyang’anyiro cha Urais kwa tiketi ya CCM na Rais Mteule Dkt John Pombe Joseph Magufuli mara baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva kutangaza kutangaza rasmi matokeo ya uchaguzi mkuu Ikulu jijini Dar es salaam ambako walifuatilia kwa pamoja matangazo hayo ya moja kwa moja kupitia vituo vya televisheni jioni hii Oktoba 29, 2015
Mama Salma Kikwete akimpongeza rais mteule
wananchi wakishangilia ushindi wa dkt Magufuli

Thursday 29 October 2015

ASEMAVYO PROFESA LIPUMBA BAADA YA KUFUTWA MATOKEO UCHAGUZI ZANZIBAR

KWA HALI ILIVYO, BORA TURUDI HUKOOOOOO......

MATOKEO RASMI URAIS (CCM NA CHADEMA) KWA MAJIMBO YALIYO TAYARI KUWAKILISHA

1. URAIS Jimbo TEMEKE
CCM: 106,612
CHADEMA: 124,274

2. URAIS Jimbo RUFIJI
CCM - 21,714
CHADEMA - 18,308

3. URAIS Jimbo KIBITI
CCM: 21,142
CHADEMA: 18,629

4. URAIS Jimbo MBARALI
CCM: 55,933
CHADEMA: 45,374

5. URAIS Jimbo BARIADI
CCM: 85,813
CHADEMA: 57,922

6. URAIS Jimbo GEITA MJINI
CCM - 43,576
CHADEMA - 25,030

7. URAIS Jimbo UBUNGO
CCM: 71,928
CHADEMA: 83,637

8. URAIS Jimbo BUSOKELO
CCM: 18,834
CHADEMA: 12,596

9. URAIS Jimbo KWELA
CCM: 49,196
CHADEMA: 32,980

10. URAIS Jimbo MOROGORO KUSINI
CCM: 35,505
CHADEMA: 13,586

11. URAIS Jimbo KARAGWE
CCM: 62,159
CHADEMA: 41,676

12. URAIS Jimbo MUHEZA
CCM: 53,237
CHADEMA: 22,635

13. URAIS Jimbo ILALA
CCM: 37,329
CHADEMA: 36,330

14. JimboBUBUBU
CCM: 10,026
CHADEMA: 7,332

15. RAIS Jimbo TABORA MJINI
CCM: 52,906
CHADEMA: 30,027

16. URAIS Jimbo ARUMERU MASHARIKI
CCM: 31,040
CHADEMA: 88,912

17. URAIS Jimbo NYAMAGANA
CCM: 99,890
CHADEMA: 78,329

18. URAIS Jimbo MTWARA MJINI
CCM: 25,828
CHADEMA: 30,195

19. URAIS Jimbo BUKOBA VIJIJINI
CCM: 64,839
CHADEMA: 32,346

20. URAIS Jimbo SONGWE
CCM: 30,778
CHADEMA: 14,738

21. URAIS Jimbo CHEMBA
CCM: 51,594
CHADEMA: 20,800

22. URAIS Jimbo BUCHOSA
CCM: 62,762
CHADEMA: 31,660

23. URAIS Jimbo KILWA KASKAZINI
CCM: 17,553
CHADEMA:14,722

24. URAIS Jimbo KIBAKWE
CCM: 36,830
CHADEMA: 8,018

25. URAIS Jimbo KILWA KUSINI
CCM: 18,767
CHADEMA: 22,377

26. URAIS Jimbo MOROGORO KUSINI MASHARIKI
CCM: 30,624
CHADEMA: 13,304

27. URAIS Jimbo HANANG
CCM: 63,205
CHADEMA: 32,367

28. URAIS Jimbo MOROGORO MJINI
CCM: 85,440
CHADEMA: 65,580

29. URAIS Jimbo KIGAMBONI
CCM: 35,735
CHADEMA: 39,754
====================================
October 28, 2015 - Saa 4 Asubuhi

Jimbo la Lupa-Mbeya

Magufuli (CCM):37,684
Lowassa (CHADEMA): 20,175

Jimbo la Lushoto-Tanga

Magufuli (CCM):28,058
Lowassa (CHADEMA): 8,673

Jimbo la Musoma Mjini-Mara

Magufuli (CCM):33,658
Lowassa (CHADEMA): 25,352

Jimbo la Mvomero-Morogoro

Magufuli (CCM): 68,179
Lowassa (CHADEMA):33,468

Jimbo la Hai-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 29,341
Lowassa (CHADEMA):49,125

Jimbo la Bukombe-Geita

Magufuli (CCM):50,063
Lowassa (CHADEMA): 28106

Jimbo la Iringa Mjini

Magufuli (CCM): 36,584
Lowassa (CHADEMA):38,860

Jimbo la Bagamoyo

Magufuli (CCM):29,969
Lowassa (CHADEMA):16,245

Jimbo la Sumbawanga mjini-Rukwa

Magufuli (CCM):43,542
Lowassa (CHADEMA): 34,201


Jimbo la Same Mashariki-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 18,520
Lowassa (CHADEMA):17,874

Jimbo la Mlalo
Magufuli (CCM): 33,996
Lowassa (Chadema): 8,938

Jimbo la Kishapu
Kura:86,125
Magufuli (CCM):65,173
Lowassa (Chadema):17,177

Jimbo la Msalala
Kura:64,111
Magufuli(CCM):44,213
Lowassa (Chadema):16,942

Jimbo la Ludewa
Kura: 48,499
Magufuli (CCM):35,365
Lowassa (Chadema):11,715

Jimbo la Tarime Mjini
Kura: 35,060
Magufuli(CCM): 18,009
Lowassa (Chadema): 15,992

Jimbo la Mtwara Vijijini
Kura: 51,233
Magufuli (CCM):25,938
Lowassa (Chadema):24,518

Jimbo la Busanda
Kura:114,955
Magufuli(CCM):73,834
Lowassa (Chadema):35,373

Jimbo la Ushetu
Kura: 76,757
Magufuli (CCM):51,034
Lowassa (Chadema):21,585

Jimbo la Shinyanga Mjini
Kura:68,745
Magufuli (CCM): 41,692
Lowassa (Chadema):25,465

Jimbo la Mbogwe
Kura: 58,837
Magufuli (CCM):44,558
Lowassa (Chadema):12,040

Jimbo la Kasulu Mjini
Kura: 52,670
Magufuli (CCM): 32,297
Lowassa (Chadema): 15,762

Jimbo la Mlimba
Kura:76,182
Magufuli (CCM): 39,555
Lowassa (Chadema):35,994

Jimbo la Mikumi
Kura: 65,241
Magufuli(CCM):35,192
Lowassa (Chadema):26,841

Jimbo la Kilosa
Kura: 83,679
Magufuli (CCM):55,839
Lowassa (Chadema):24,276

Jimbo la Bukoba Mjini
Kura: 53,710
Magufuli (CCM): 27,620
Lowassa (Chadema): 25,898

Jimbo la Moshi Vijijini
Kura: 82,782
Magufuli (CCM): 25,017
Lowassa (Chadema): 54,823

Jimbo la Sengerema
Kura:104108
Magufuli (CCM):69392
Lowassa (Chadema):28335

Matokeo ya Urais, Jimbo la Tunduma
Kura:52,797
Magufuli (CCM):19,446
Lowassa (Chadema):32,219

Matokeo ya Urais, Mufindi Kaskazini
Kura:36,076
Magufuli(CCM):26,412
Lowassa (Chadema):8,085

Matokeo ya Urais, Jimbo la Nysa
Kura: 46,551
Magufuli(CCM):30,609
Lowassa (Chadema):14,062

Matokeo ya Urais, Jimbo la Isimani
Kura:42,933
Magufuli(CCM):26,766
Lowassa (Chadema):15,303

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kavuu
Kura: 30,813
Magufuli (CCM): 21,483
Lowassa (Chadema): 8,083

Matokeo ya Urais, Mpanda Mjini
Kura: 50,623
Magufuli(CCM): 32,770
Lowassa (Chadema): 16,569

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kalenga
Kura:58,932
Magufuli (CCM):40,896
Lowassa (Chadema):16,890

Matokeo ya Urais, Jimbo la Rombo
Kura:82,862
Magufuli (CCM): 21,908
Lowassa (Chadema): 57,715

Matokeo ya Urais, Kahama Mjini
Kura: 89,961
Magufuli(CCM): 58,728
Lowassa (Chadema): 27,501

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kwimba
Kura: 53,760
Magufuli(CCM):40,544
Lowassa (Chadema):10,071

Matokeo ya Urais, Jimbo la Magu
Kura: 105,804
Magufuli(CCM):69,991
Lowassa (Chadema):30,070

Matokeo ya Urais, Jimbo la Geita
Kura: 69,778
Magufuli(CCM): 45,472
Lowassa (Chadema):18,640

Matokeo ya Urais, Jimbo la Chato
Kura: 117,485
Magufuli(CCM):83,820
Lowassa (Chadema):27,936

Matokeo ya Urais, Jimbo la Bahi
Kura: 67,993
Magufuli (CCM): 51,138
Lowassa (Chadema): 11,340

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kilombero
Kura:99,255
Magufuli(CCM):49478
Lowassa (Chadema):49166

Matokeo ya Urais, Mbinga Vijijini
Kura: 72,545
Magufuli (CCM):55,895
Lowassa (Chadema):12,213

Matokeo ya Urais, Jimbo la Sumve
Kura: 46,293
Magufuli (CCM): 32,079
Lowassa (Chadema):11,203

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kalambo
Kura:70,575
Magufuli(CCM):38,165
Lowassa (Chadema):29,507

Matokeo ya Urais, Jimbo la Busega
Kura:70,664
Magufuli (CCM):47,049
Lowassa (Chadema):19,765

Matokeo ya Urais, Jimbo la Kilolo
Kura: 82,079
Magufuli (CCM):52,517
Lowassa (Chadema):25,424

Matokeo ya Urais, Jimbo la Gairo
Kura: 54,157
Magufuli (CCM): 44,659
Lowassa (Chadema):6,925

Matokeo ya Urais, Jimbo la Liwale
Kura: 44360
Magufuli(CCM):19,967
Lowassa (Chadema): 23,176

===========================================
October 27, 2015 - Saa 2 Usiku

Jimbo la Mfenesini-Mjini Magharinibi

Magufuli (CCM): 4496
Lowassa (CHADEMA): 3047

Jimbo la Mahonda

Magufuli (CCM): 4760
Lowassa (CHADEMA): 1449

Jimbo la Rungwe-Mbeya

Magufuli (CCM): 47,862
Lowassa (CHADEMA):41,534

Jimbo la Arumeru Magharibi-Arusha

Magufuli (CCM): 27,658
Lowassa (CHADEMA): 105,720

Jimbo la Pangani-Tanga

Magufuli (CCM):14,041
Lowassa (CHADEMA): 10,151

Jimbo la Korogwe Vijijini-Tanga

Magufuli (CCM): 51,984
Lowassa (CHADEMA):19,050

Jimbo la Kijito Upele-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 8,075
Lowassa (CHADEMA):5,639

Jimbo la Chahali-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 4689
Lowassa (CHADEMA):2585

Jimbo la Kiembe Samaki

Magufuli (CCM): 6618
Lowassa (CHADEMA): 5610

Jimbo la Chahali-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 4689
Lowassa (CHADEMA):2585

Jimbo la Manyoni Magharibi-Singida

Magufuli (CCM): 24,675
Lowassa (CHADEMA): 9901

Jimbo la Iramba Magharibi-Singida

Magufuli (CCM): 50,322
Lowassa (CHADEMA):11,714

Jimbo la Dimani-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 5,292
Lowassa (CHADEMA): 1,861

Jimbo la Nzega-Tabora

Magufuli (CCM): 18,843
Lowassa (CHADEMA):10,195

Jimbo la Igunga-Tabora

Magufuli (CCM): 36,796
Lowassa (CHADEMA):18,600

Jimbo la Urambo Mashariki-Tabora

Magufuli (CCM): 36,458
Lowassa (CHADEMA): 22,385

Jimbo la Babati Vijijini-Manyara

Magufuli (CCM): 67,183
Lowassa (CHADEMA): 42,334

Jimbo la Kiteto-Manyara

Magufuli (CCM): 41,862
Lowassa (CHADEMA): 31,268

Jimbo la Bukene-Tabora

Magufuli (CCM):36,229
Lowassa (CHADEMA): 11,380

Jimbo la Sikonge-Tabora

Magufuli (CCM): 36,729
Lowassa (CHADEMA):16,164

Jimbo la Kaliua-Tabora

Magufuli (CCM): 28,599
Lowassa (CHADEMA): 19,724

Jimbo la Ulyankulu-Tabora

Magufuli (CCM): 35,329
Lowassa (CHADEMA):7,568

Jimbo la Kyela-Mbeya

Magufuli (CCM): 44,451
Lowassa (CHADEMA):37,563

Jimbo la Manonga-Tabora

Magufuli (CCM):32,013
Lowassa (CHADEMA): 14,343

Jimbo la Ukerewe-Mwanza

Magufuli (CCM): 55,091
Lowassa (CHADEMA):47,667

Jimbo la Dodoma-Mpwapwa

Magufuli (CCM):37,480
Lowassa (CHADEMA):8,230

Jimbo la Longido-Arusha

Magufuli (CCM):14,621
Lowassa (CHADEMA): 25,361

Jimbo la Kondoa Mijini-Dodoma

Magufuli (CCM):15,113
Lowassa (CHADEMA): 7,102

===================================
October 27, 2015 - Saa 8.40 Mchana

Jimbo la Fuoni-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 956
Lowassa (CHADEMA):420

Jimbo la Kikwajuni-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6,317
Lowassa (CHADEMA): 3669

Jimbo la Mpanda Vijijini-Katavi

Magufuli (CCM):37,321
Lowassa (CHADEMA): 12,791

Jimbo la Mchinga-Lindi

Magufuli (CCM):13,948
Lowassa (CHADEMA):12,936

Jimbo la Mwela-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6430
Lowassa (CHADEMA):5865

Jimbo la Nkasi Kaskazini-Rukwa

Magufuli (CCM):25,837
Lowassa (CHADEMA):19,891

Jimbo la Nkasi Kusini-Rukwa

Magufuli (CCM): 21,572
Lowassa (CHADEMA): 13,550


Jimbo la Nkenge-Kagera

Magufuli (CCM): 42,568
Lowassa (CHADEMA): 25,840

Jimbo la Amani-Kusini Magharibi

Magufuli (CCM):4,322
Lowassa (CHADEMA):3,157

Jimbo la Bumbwini

Magufuli (CCM):2503
Lowassa (CHADEMA): 2822

Jimbo la Nungwi- Mkoa wa Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM):4135
Lowassa (CHADEMA): 4853

Jimbo la Uzini

Magufuli (CCM):6537
Lowassa (CHADEMA):1864

Jimbo la Chwaka

Magufuli (CCM):6537
Lowassa (CHADEMA): 1864

Jimbo la Mtama-Lindi

Magufuli (CCM):29,625
Lowassa (CHADEMA):20,841

Jimbo la Tunguu-Kusini Unguja

Magufuli (CCM): 8,519
Lowassa (CHADEMA): 2,923

Jimbo la Biharamuro-Kagera

Magufuli (CCM):44,943
Lowassa (CHADEMA):28,576

Jimbo la Arusha Mjini-Arusha

Magufuli (CCM): 65,107
Lowassa (CHADEMA): 150,786

Jimbo la Chake Chake

Magufuli (CCM):1253
Lowassa (CHADEMA):5209

Jimbo la Kibaha Vijijini-Pwani

Magufuli (CCM):20,805
Lowassa (CHADEMA):11,344

Jimbo la Mwanakwereke

Magufuli (CCM): 4206
Lowassa (CHADEMA):4606

Jimbo la Nachingwea-Lindi

Magufuli (CCM):46,485
Lowassa (CHADEMA):30,252

Jimbo la Mafya- Pwani

Magufuli (CCM): 11,153
Lowassa (CHADEMA):9,363

Jimbo la Mkuranga- Pwani

Magufuli (CCM):45,710
Lowassa (CHADEMA): 36,478

Jimbo la Welezo

Magufuli (CCM):2615
Lowassa (CHADEMA):2582

Jimbo la Magomeni-Kusini Magharibi

Magufuli (CCM): 5716
Lowassa (CHADEMA):3711
== ===================================
October 27, 2015 - Saa 3 Asubuhi

Jimbo la Chalinze

Magufuli (CCM):52,212
Lowassa (CHADEMA):21380

Jimbo la Chonga

Magufuli (CCM):1740
Lowassa (CHADEMA):3800

Jimbo la Chumbuni

Magufuli (CCM): 5096
Lowassa (CHADEMA): 4450

Jimbo la Ileje

Magufuli (CCM):26,368
Lowassa (CHADEMA): 15,651

Jimbo la Kijini

Magufuli (CCM): 2703
Lowassa (CHADEMA): 3351

Jimbo la Kilindi-Tanga

Magufuli (CCM): 33,942
Lowassa (CHADEMA):12,123

Jimbo la Korogwe Mjini-Tanga

Magufuli (CCM): 17,168
Lowassa (CHADEMA): 9034

Jimbo la Kohani-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6,245
Lowassa (CHADEMA): 2689


Jimbo la Lupembe-Njombe

Magufuli (CCM): 23,061
Lowassa (CHADEMA): 7,466

Jimbo la Madaba-Ruvuma

Magufuli (CCM): 13,949
Lowassa (CHADEMA):4,735

Jimbo la Masasi Mjini-Mtwara

Magufuli (CCM): 24,637
Lowassa (CHADEMA):16,778

Jimbo la Mbeya Vijijini-Mbeya

Magufuli (CCM):62,662
Lowassa (CHADEMA):47,038

Jimbo la Mkwajuni-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 4,686
Lowassa (CHADEMA): 3,314

Jimbo la Momba- Mbeya

Magufuli (CCM): 28,978
Lowassa (CHADEMA):24,418

Jimbo la Monduli-Arusha

Magufuli (CCM):11,355
Lowassa (CHADEMA): 49,675

Jimbo la Mpendae- Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):4,192
Lowassa (CHADEMA): 4,048

Jimbo la Mwanga-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 25,738
Lowassa (CHADEMA):15,148

Jimbo la Namtumbo-Ruvuma

Magufuli (CCM):44,061
Lowassa (CHADEMA): 23,039

Jimbo la Newala Mjini-Mtwara

Magufuli (CCM): 21,269
Lowassa (CHADEMA):16,980

Jimbo la Newala Vijijini-Mtwara

Magufuli (CCM): 29,799
Lowassa (CHADEMA): 13,958

Jimbo la Siha-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 18,252
Lowassa (CHADEMA):22,572

Jimbo la Solwa-Shinyanga

Magufuli (CCM): 66,096
Lowassa (CHADEMA): 23,510

Jimbo la Tandahimba

Magufuli (CCM): 49,098
Lowassa (CHADEMA):46,288

Jimbo la Tumbatu-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 5,720
Lowassa (CHADEMA): 3,967

Jimbo la Igalula-Tabora

Magufuli (CCM): 28,747
Lowassa (CHADEMA): 8,393

Jimbo la Ulanga-Morogoro

Magufuli (CCM):32,297
Lowassa (CHADEMA):20,489

Jimbo la Wawi-Kusini Pemba

Magufuli (CCM): 1,748
Lowassa (CHADEMA): 5,216

Jimbo la Ziwani-Kusini Pemba

Magufuli (CCM): 592
Lowassa (CHADEMA):6,067

Jimbo la Ole-Kusini Pemba

Magufuli (CCM):681
Lowassa (CHADEMA):5,251

Jimbo la .....-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 5,592
Lowassa (CHADEMA): 1,019

Jimbo la Tabora Kaskazini-Tabora

Magufuli (CCM): 38,050
Lowassa (CHADEMA): 12,410

Jimbo la Ruangwa

Magufuli (CCM): 34,516
Lowassa (CHADEMA): 26,827

Jimbo la Malindi-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 2,581
Lowassa (CHADEMA): 5,662

Jimbo la Jang'ombe-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 6,567
Lowassa (CHADEMA):2,839

Jimbo la Mhambwe-Kigoma

Magufuli (CCM): 37,746
Lowassa (CHADEMA): 22,804

===============================
Oktoba 26, 2015 - Saa 4 asubuhi:

Jimbo la Makunduchi:

Magufuli (CCM): 8,406
Lowassa (CHADEMA): 1,769

Jimbo la Paje:

Magufuli (CCM): 6,035
Lowassa (CHADEMA): 1,899

Jimbo la Lulindi:

Magufuli (CCM): 31,603
Lowassa (CHADEMA): 11,543

October 26, 2015 - Saa 11 Jioni
Jimbo la Mkoani:

Magufuli (CCM): 3341
Lowassa (CHADEMA): 7368

Jimbo la Ndanda:

Magufuli (CCM): 33699
Lowassa (CHADEMA): 19017

Jimbo la Kiwengwa:

Magufuli (CCM): 3317
Lowassa (CHADEMA): 1104

Jimbo la Nsimbo:

Magufuli (CCM): 31413
Lowassa (CHADEMA): 6042

Jimbo la Mtambile:

Magufuli (CCM): 902
Lowassa (CHADEMA): 5875

Jimbo la Donge:

Magufuli (CCM): 5592
Lowassa (CHADEMA): 1019

Jimbo la Kiwani:

Magufuli (CCM): 1661
Lowassa (CHADEMA): 4229

Jimbo la Chambani:

Magufuli (CCM): 818
Lowassa (CHADEMA): 5319

Jimbo la Kibaha Mjini:

Magufuli (CCM): 34604
Lowassa (CHADEMA): 25448

Jimbo la Bumbuli:
Magufuli (CCM): 35310
Lowassa (CHADEMA): 7928

October 26, 2015 - Saa 2 Usiku
Jimbo la Gando:

Magufuli (CCM): 881
Lowassa (CHADEMA): 5903

Jimbo la Kisarawe:

Magufuli (CCM): 24086
Lowassa (CHADEMA): 13093

Jimbo la Kojani:

Magufuli (CCM): 1561
Lowassa (CHADEMA): 9982

Jimbo la Mbinga Mjini:

Magufuli (CCM): 29295
Lowassa (CHADEMA): 11695

Jimbo la Mgogoni:

Magufuli (CCM): 710
Lowassa (CHADEMA): 6506

Jimbo la Mkinga:

Magufuli (CCM): 23798
Lowassa (CHADEMA): 15142

Jimbo la Moshi Mjini:

Magufuli (CCM): 28909
Lowassa (CHADEMA): 49379

Jimbo la Mtambwe:

Magufuli (CCM): 428
Lowassa (CHADEMA): 6937

Jimbo la Nanyamba:

Magufuli (CCM): 24904
Lowassa (CHADEMA): 16992

Jimbo la Peramiho:

Magufuli (CCM): 32505
Lowassa (CHADEMA): 11291

Jimbo la Wete:
Magufuli (CCM): 958
Lowassa (CHADEMA): 5119

Jimbo la Singida Mjini

Kura: 56,558

Magufuli (CCM): 36,035

Edward Lowassa (Chadema): 19,007

Jimbo la Lindi Mjini
Kura: 38,992
Magufuli (CCM): 21,088
Edward Lowassa(Chadema): 17,607

Jimbo la Njombe Mjini
Kura: 55,772
Magufuli (CCM): 33,626
Edward Lowassa(Chadema):20,368

Tuesday 27 October 2015

MATOKEO YA UCHAGUZI YAANZA KUTANGAZWA

Jimbo la Sumbawanga Mjini: Aeshi Hilaly wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 41763, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Ikuwo Malila wa Chadema, aliyepata kura 36183

Joram Hongoli wa Chama cha Mapinduzi (CCM) atangazwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Lupembe kwa kupata jumla ya kura 20,430 na kumwangusha mpinzani wake toka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Edwin Swalle aliyepata jumla ya kura 10407.

Jimbo la Mchinga: Hassan Bobali wa CUF, ameshinda kwa jumla ya kura 14776, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Saidi Mtanda wa CCM, aliyepata kura 13665

Jimbo la Singida Magharibi: Kingwi Immanuel wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 25102, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Allute Mdinka wa Chadema, aliyepata kura 13480

Jimbo la Singida Mashariki: Tundu Lissu wa Chadema, ameshinda kwa jumla ya kura 25010, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Jonathan Njau wa CCM, aliyepata kura 18614.‪

Jimbo la Singida Mjini: Mussa Sima wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 36690, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Mgana Msindai wa Chadema, aliyepata kura 16702

Wiliiam Lukuvi atangazwa kuwa mshindi kwa kiti cha Ubunge toka tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Ismani, mkoani Iringa kwa kuwa na jumla ya kura 26,119 na mpinzani wake Patrick Sosopi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kushindwa kwa kupata jumla ya kura 15,534

Jimbo la Mtama: Nape Nnauye wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 28110, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Suleiman Luwongo wa Chadema, aliyepata kura 13918

Cecil Mwambe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) apata kiti cha Ubunge katika Jimbo la Ndanda mkoani Mtwara kwa kuwa na kura 26,247, huku Mariam Kasembe wa Chama cha Mapinduzi kukikosa kiti hiko kwa kupata kura 26,215

Jimbo la Same Magharibi: Dkt. David Mathayo wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 21418, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Christopher Sangweli wa Chadema, aliyepata kura 15347
Jimbo la Same Mashariki:Naghenjwa Livingstone Kaboyoka wa Chadema, amembwaga Anne Kilango Malecela kwa jumla ya kura 18836, dhidi ya kura 15539.‪

Jimbo la Mbogwe: Augustino Manyanda wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 32921, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Maganga Nicodemas Henry wa Chadema, aliyepata kura 13975.

Mtwara mjini Maftah Nachuma wa Chama cha CUF ameshinda kwa kura za Ubunge, huku Asnain Murji kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) ashindwa kukitetea kiti chake

Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Freeman Mbowe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) atangazwa kuwa Mbunge kwa kupata jumla ya kura 51,124, huku mgombea kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Danstan Mallya apata jumla ya kura 26,966.

Jimbo la Ngara: Alex Gashaza wa CCM, ameshinda kwa jumla ya kura 53387, dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Dkt.Peter Bujari wa Chadema aliyepata kura 35254

Jimbo la Mbeya Mjini: Joseph Mbilinyi wa Chadema, ameibuka mshindi kwa jumla ya kura 97675, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Mwalyego Shitambala wa CCM, aliyepata kura 46894

Jimbo la Iramba Magharibi: Mwigulu Nchemba wa CCM, aibuka mshindi kwa jumla ya kura 55213, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Jesca Kishoa wa Chadema aliyepata kura 12957

Jimbo la Ileje: Janet Mbene wa CCM, aibuka mshindi kwa jumla ya kura 27582, dhidi ya mpinzani wake wa karibu Emmanuel Mbuba wa NCCR-Mageuzi, aliyepata kura 14578.

Jimbo la Mpanda Mjini: Sebastian Kapufi wa CCM, aibuka mshindi kwa jumla ya kura 29193, dhidi ya mpinzani wake wa karibu wa Chadema Jonas Kalinde, aliyepata kura 18649

Sunday 25 October 2015

Saturday 24 October 2015

MGOMBEA MWENYE HOFU YA MUNGU

\
HISTORIA ya maisha yake tangu alipozaliwa hadi sasa, John Pombe Magufuli ameishi katika matakwa ya dini ya Kikrosto.

Mbali na kuwa mkristo, mkatoliki, anamheshimu kila mtu. Mwenye imani kama yake, imani tofauti na hata wale wasio na dini, wote anawapa haki sawa. Amemtanguliza Mungu katika kila jambo. Safari yake ya kuomba urais, aliianza kwa kumtanguliza Mungu na kweli akajibu maombi yake. Kumbuka katika safari hiyo kulikuwa na watu 42 waliokuwa wakiwania nafasi hiyo, kila mmoja aliomba kwa imani yake lakini Mungu akamuongoza Mugufuli, akapitishwa.
Mchakato wake wa kutangaza nia ulikuwa wa kimyakimya. Hakutoa ruswa kwa mtu yeyote ili aipate nafasi hiyo japo baadhi ya wenzake walidaiwa kutoa ili waweze kupitishwa na vikao vya chama.

Tangu akiwa shule ya msingi, Magufuli aliishi maisha ya kumpendeza Mungu licha ya kukutana na changamoto mbalimbali zilizosababishwa na ukata.

Alitembea umbali wa kilometa 5 kila siku kutoka kijiji cha Rubambangwe hadi Shule ya Msingi Chato. Hakuwahi kuchelewa. Alikuwa ni mtu wa kujituma, hakupenda kukwazana na mtu. Zaidi alizingatia masomo yake ya kemia na baadaye kuwa mtaalamu aliyebobea katika masomo hayo.

Mwalimu wake, marehemu Cornely Pastory aliwahi kueleza dhahiri kwamba, Magufuli ni miongoni mwa wanafunzi wake waliokuwa wapole, wanyenyekevu ambao hawakuwa na historia mbaya shuleni. Aliiishi kwa matakwa ya Mungu.

Historia yake kimaisha imeendelea kuwa hivyo. Hakuwa mtu wa kujikweza hata alipokuwa waziri. Mke wake aliendelea kuwa mwalimu wa shule msingi. Watoto wake amewalea katika maadili ya dini, amekuwa mzalendo na ndiyo maana hakuna mwanaye hata mmoja aliyekwenda kusoma nje ya nchi kuanzia hatua ya awali hadi chuo kikuu.

Huyo ndiye Magufuli ambaye kwa macho ya kawaida kabisa unaona anatosha kuwa rais. Mahali popote amekuwa akimtanguliza Muingu katika majukumu yake. Baada ya Mungu, anatekeleza sheria ili asimuonee mtu.

Amekuwa akisimamia sheria katika barabara. Tumeshuhudia akivunja nyumba ambazo zimeifuata barabara bila kujali ni ya nani. Anasimamia sheria, hatishwi na tajiri. Anaangalia sheria inasema nini, kama amepindisha basi anapambana naye.

Hofu ya Mungu ndiyo inayomuongoza kusimamia sheria. Anachukia ufisadi na rushwa. Akiwa Wizara ya Ujenzi, amewatimua wafanyakazi wengi wala rushwa. Anatamani kila mmoja ale kulingana na haki yake.

Alipokuwa akihutubia kwenye Uwanja wa Jangwani jijini Dar katika uzinduzi wa kampeni zake, alianza kwa kumtanguliza Mungu mbele. Aliwashukuru Watanzania wote waliojitokeza uwanjani hapo kwa kumuamini, hakumbagua mtu kwa dini, kabila lakini zaidi aliwasalimu katika jina la Mungu.

“Ningependa kushughulika na uchumi wetu, ukue. Kila mmoja wetu awe na uchumi mzuri hususan kwa wanyonge, natamani zaidi niwasaidie hao,” alisema Magufuli kwenye mkutano huo.

Aidha, kwenye hotuba hiyo, Magufuli alitumia muda mrefu zaidi kuwazungumzia Watanzania wa hali ya chini. Hivyo ndivyo alivyokuwa akizungumza katika mikutano yake mingi. Amekuwa akisema matatizo ya Watanzania anayajua.

Aliposema anayajua alimaanisha kwani alieleza wazi kwamba ameyaishi. Amechunga ng’ombe kama wachungaji wengi wa kawaida. Hivyo atafanya kila linalowezekana kuhakikisha anamaliza tatizo la umasikini.

Akaendelea mbele zaidi kwa kuwaahidi Watanzania kwamba anatambua nchi ina watu wenye imani tofauti hivyo wote watakuwa na haki sawa, matatizo yote atayatatua pasipo kujalia itikadi za kivyama, ukabila wala udini.

Magufuli alisisitiza amani. Akazungumzia kudumisha umoja miongoni mwa Watanzania. Alipohamia mikoani, Magufuli alionekana kumtanguliza Mungu katika kila anachokifanya. Aliomba Watanzania wampe kazi ya urais ili awatumikie.

Alieleza sera zake huku akihofia kumdanganya mtu. Alikataa uongo kwani ni dhambi. Alitamka ahadi ambazo anaamini zinatekelezeka.

Kile ambacho aliona hakitekelezeki kutekeleza, alisema dhahiri huku akionesha juhudi za kupatia ufumbuzi.

“Ndugu zangu mimi nasema ukweli. Nasema ukweli kutoka moyoni, nikiahidi kitu lazima nitekeleze. Kwangu mimi ni kazi tu. Siwezi nikasema nitamaliza nyumba zote za tembe nchi nzima kwa wakati mmoja. Huo utakuwa ni uongo. Wanaosema hivyo ni waongo. Tutazipunguza kwa awamu na nina imani ipo siku zitakwisha kabisa,” alisema Magufuli katika moja ya mikutano yake ya kampeni.

Kwenye kipindi cha kampeni, wagombea mbalimbali wamekuwa wakitoa ahadi ambazo ukizitathimini kwa jicho la tatu hazitekelezeki. Kwa Magufuli hilo halipo, yeye amekuwa akiahidi ahadi ambazo anaamini zinatekelezeka.

Hakutaka kuonekana muongo. Hakutaka kutenda dhambi hiyo na ndiyo maana kila alipopita amesisitiza Watanzania wamuombee ili aweze kuifanya kazi ya urais katika matakwa ya Mungu.

“Ndugu zangu nimeomba kazi hii ya urais nikiamini naiweza. Nikiwatazama hapa mlivyokusanyika, mnadhihirisha kwamba mnanipenda. Ndugu zangu mniombee...”-Magufuli.

Ameyasema hayo huku machoni akionesha anamaanisha. Hiyo imemuongezea imani kubwa Magufuli kwa Watanzania. Akizungumzia umasikini anaonekana anaguswa na tatizo hilo, ana kiu ya kutaka kulitatua.

Mungu ni upendo, Magufuli anahiza amani, umoja kwa Watanzania wote kwa sababu ana hofu ya Mungu, huyo ndiye rais mtarajiwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!







USHAURI

CCM YAFUNGA KAMPENI JANGWANI

Ikiwa imesalia siku moja kabla ya uchaguzi,jana CCM ilifanya mkutano mkubwa wa kapeni Jangwani Dar na leo hivi Dk magufuli atakuwa Kirumba Mwanza
Mke wa Rais mama Salma Kikwete akiteta jambo na mke wa Mgombea urais CCM Mama Janeth magufuli katika Viwanja vya Jangwani Jijini dar

Friday 23 October 2015

RAIS KIKWETE AONGEA NA WANANCHI WA DAR

MAKAMANDA KATIKA UBORA WAO

VIDEO: MAGUFULI ANAVYOKERWA WANANCHI KUNYANYASIKA

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU: BAA NA CLUB ZA USIKU ZAPEWA MSIMAMO

Serikali jijini Dar es Salaam imeagiza baa zote zinazouza pombe mpaka asubuhi kusitisha shughuli hiyo mkesha wa siku ya uchaguzi ili kuimarisha usalama Jumapili ijayo.

Aidha, imesisitiza kwamba kila mwananchi atakayekwenda kupiga kura ahakikishe anarudi nyumbani baada ya shughuli hiyo badala ya kukaa katika vikundi kusubiri matokeo vituoni.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, katika ibada maalum ya kuliombea Taifa amani na mvua, iliyoendeshwa na Askofu Charles Gadi wa Kanisa la Huduma ya Good News for All Ministry, jijini Dar es Salaam juzi.

Askofu Gadi katika maombi yake alisisitiza suala la amani na kumuomba Mwenyezi Mungu alete mvua ili mabwawa yanayozalisha umeme yajae maji nishati ya umeme ipatikane nchini kwa uhakika.

Thursday 22 October 2015

BISHENI/KATAENI TENA

Hiyo inaitwa amsha amsha........
Maneno tata ya viongozi wa Ukawa