Saturday 31 December 2016

MWAKA MPYA ULEEEEEEEEE

TAHADHARI: KWA JOTO HILI .......

Jamani naomba nitoe tahadhari.
Jua limekuwa kali mno na joto kuongezeka sana hasa Dar na kwingineko..viumbe hai vinahangaika makazi hayakaliki...nyoka, nge, tandu ambao si rahisi kuwasikia wanatembea au kutambaa au hata kuwaona wakiwa mbali, wanatafuta maeneo tofauti ya kujihifadhi na hasa kupenya kwenye makazi..nyumba zetu. Mnatahadharishwa kuhakikisha milango na madirisha vimefungwa vema wakati wote kuzuia wasipenye..nyumba zipigwe dawa ndani na nje. jua ni kali na maeneo mengi yana ukame kipindi hiki.

Hii picha ya mamba ni ya leo leo pande za Kigamboni Mwongozo ,amekutwa akizagaa kitaa wananch wakamshughulkia

Friday 30 December 2016

2017 BEI YA UMEME KUPANDA

Bei za umeme zimepanda kwa 8.5% badala ya 18.19% iliyopendekezwa na TANESCO.

Ongezeko la bei ya huduma za umeme limetokana na kuzidi kwa gharama za uzalishaji wake.

Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) ambalo linanunua umeme wa jumla kupeleka Zanzibar limeongezewa 5.7% ya bei ya umeme.

Ongezeko hilo halitaathiri wateja wa majumbani ambao matumizi yao hayazidi uniti 75 kwa mwezi.

Kundi la TIb linalohusisha viwanda vidogo,mabango na minara ya mawasiliano litakua na tozo ya mwezi ya shilingi 5,520.

Bei hizo zitaanza kutumika Januari Mosi mwaka 2017.

TANESCO inatarajia kufanya maboresho ya msongo wa umeme na kutekeleza miradi mipya ya kuunganisha wateja ili kuboresha huduma za umeme.

IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO)

ENZI ZA MWALIMU.......


KINADADA MWAKA 2017 PUNGUZENI MADOIDO

Hapa nani kamuiga nani, tuwe wakweli?

Wednesday 28 December 2016

MAAMUZI YA RUFAA YA KESI YA MHE GODBLESS LEMA KUJULIKANA JAN 4,2017

Na.Vero Ignatus Arusha.
Mahakama kuu kanda ya Arusha imesikiliza maombi ya rufaa yayaliyowasilishwa na upande wa jamhuri na ule wa mshtakiwa Godbless Lema ambapo pande zote mbili wamekubaliana kusikilizwa rufaa ya upande wa jamhuri ambapo upande wa serikali wameiomba mahakama kuwasilisha kwa hati ya maandishi hapo kesho tarehe 30 disemba 2016
Aidha rufaa hizo ni pamoja na ile ya upande wa Jamhuri kutoridhika na maamuzi ya Jaji Dkt. Modesta Opiyo la kuwapa siku kumi (10) upande wa mshtakiwa Lema kufaili notisi ya rufaa ,na upande wa mshtakiwa ni ile ya kupinga uamuzi wa mahakama ya chini kushindwa kumpa Lema masharti ya dhamana
Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi ya rufaa hizo Salma Magimbi amesema kuwa mara baada ya upande wa jamhuri kuleta rufaa kwa njia ya maandishi upande wa mshtakiwa Lema wataijibu tarehe 30 desemba 2016 ambapo tarehe 2 januari watakutana pande zote kwa ajili ya kufanya majumuisho na maamuzi ya rufaa hiyo yatatolewa tarehe 4 januari 2017
Hata hivyo baada ya kusikiliza rufaa hizo mahakama imeibua hoja yenyewe na kuwapa kazi mawakili wa pande zote mbili kuangalia kuwa notisi iliyowasilishwa na mahakama ya chini imekidhi matakwa ya kisheria?
Kwa upande wa wakili wa mshtakiwa Peter Kibatala amesema kuwa kwa upande wao wameiomba mahakama kusubirisha rufaa yao ili wasikilize kwanza rufaa ya upande wa jamhuri kwani rufaa zote zimegongana na zinaelekea sehemu moja
"Unajua leo rufaa mbili zimegongana ile ya upande wa jamhuri na ile ya kwetu sisi,hivyo basi sisis tumeiomba mahakama kusitisha rufaa yetui isikilizwe ile ya serikali kwanza,kwani rufaa zote zinaelekea upandemmoja ,wandege apande ndege na wa basi apande basi "alisema Kibatala.
Hata hivyo mbunge huyo wa Arusha mjini Godbless Lema amerudishwa rumande hadi hapo maamuzi yatakapotolewa na mahakama.

Tuesday 27 December 2016

UJENZI WA JULIUS NYERERE I AIRPORT WAFIKIA ASILIMIA 65

Tume ya mipango imefanya ziara katika mradi wa ujenzi wa jengo la III la abiria katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (Terminal III) jijini Dar es Salaam kwa lengo la kukagua maendeleo ya mradi huo na kuelezwa kuwa ujenzi umefikia asilimia 65.

Akitoa maelezo mbele ya timu ya wataalamu kutoka Tume ya Mipango, Meneja wa Mradi huo Mhandisi Mwanaidi Mkwizu alieleza kuwa ujenzi huo unaotekelezwa na Mkandarasi wa kampuni ya BAM kutoka Uholanzi ulioanza Juni 2013 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba Mwaka 2017.
Akielezea miundombinu ya uwanja huo, Mhandisi Mkwizu alisema kuwa uwanja huo wa kisasa una barabara ya kuruka ndege (runway) yenye urefu wa kilometa 3 na upana wa mita 60 ambapo upana unaohitajika kwa matumizi ya ndege ni mita 45.
Aliongeza kuwa mradi huo pia umeangalia changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na kuamua kutafua vyanzo mbalimbali ili kuondokana na utegemezi wa chanzo kimoja ambacho kinaweza kukwamisha shughuli katika uwanja huo pale inapotokea hitilafu.

Alieleza kuwa kutakuwa na njia mbili tofauti za kuleta umeme kutoka TANESCO ambapo njia moja ni kwa ajili ya dharura na pia endapo kutakuwa na tatizo la kukatika umeme kupitia njia za TANESCO, umeme utapatikana kutoka chanzo mbadala cha dharura kwa kutumia jenerata nne kubwa za kisasa za dizeli zilizopo eneo la mradi ambazo zinatosha kukidhi mahitaji ya eneo hilo.
Alisisitiza kuwa tayari wamefanya mazungumzo na TANESCO na kukubaliana kuwa njia hizo za umeme ni kwa ajili ya uwanja huo pekee na hakuna wateja wengine watakaounganishiwa katika njia hizo.
Mhandisi mkwizu alimalizia kwa kusema kuwa yeye pamoja na timu yake ya wataalamu wanaendelea kufanya usimamizi wa karibu ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na malengo yaliyopangwa.
Wataalamu wa ukaguzi wa miradi kutoka Tume ya Mipango walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya ujenzi wa mradi huo na kuonesha kuridhishwa na kasi yautekelezaji huku wakimshauri menejea wa mradi huo kuendelea na ufanisi wake katika kusimamia kazi hiyo ili kuhakikisha malengo ya mradi huo yanafikiwa.

UDAKU; HUYU NDIE MKE MTARAJIWA WA AY

Mwanamuziki Ay kwa mara ya kwanza amemtambulisha rasmi Mpenzi wake....
Habari hii Leo imekuwa gumzo mitandaoni kwa wengi walikuwa wakijiuliza Ay mpenzi wake ni nani hasa baada ya Swahiba wake wa Karibu Mwana FA Kuoa....

Sunday 25 December 2016

NAWATAKIA XMAS NJEMA

Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda akimuombea na kumbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Saturday 24 December 2016

KWANINI WACHAGGA WENGI HUENDA KWAO KILIMAJARO KIPINDI CHA KRISMAS?

Nimeamua kuandika kipande cha waraka huu kutokana na kuwepo kwa dhana nyingi potofu juu ya wachagga kwenda kwao kipindi cha mwisho wa mwaka, maarufu kama "kwenda kuhesabiwa".
Je ni kweli wachagga huenda kuhesabiwa? Jibu ni Hapana.. si kweli. Wachagga hawaendi kuhesabiwa.
SWALI; Sasa kama hawaendi kuhesabiwa neno "kuhesabiwa" limetoka wapi na kwanini litumike kwao tu sio kwa Wasukuma, Wamasai, Wayao au Wamakonde?

JIBU; Neno "kuhesabiwa" limetoholewa kutoka neno la Kiebrania "מִפקָד אוֹכלוּסִין" linalomaanisha Wana wa Israel kurudi kwao kwa ajili ya kuhesabiwa.

Mara nyingi Waisrael walikua wanarudi kipindi cha mwisho wa mwaka wa Kiyahudi ktk mwezi uitwao "Adar Beit" ambao kwa mujibu wa Kalenda ya Kiyahudi huo ndio mwezi wa mwisho wa mwaka. Na hukaa huko hadi mwezi wa kwanza wa mwaka ambao kwa kiyahudi huitwa "Nissan".
Utamaduni huu ulitumika ktk Israel ya zamani (Ancient Jews) japo kwa sasa haupo tena. Katika kipindi hiki Waisrael walikua wakikutana nyumbani na kupanga mipango ya maendeleo pamoja na kuhesabiwa ili kujua idadi yao kutokana na kutawanyika katika mataifa mengi duniani.
Tangu enzi za Musa miaka zaidi ya 4,000 kabla ya Kristo; Waisrael walikua na utamaduni wa kurudi kwao kuhesabiwa.

Katika kitabu cha 1 Nyakati 23:2-3 Biblia inasema "Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi. Nao wakahesabiwa Walawi wenye miaka thelathini na zaidi; na jumla yao kwa vichwa, mtu kwa mtu, ikapata thelathini na nane elfu."

Huu ni udhibitisho wa kuhesabiwa kwa Wana wa Israel zamani hizo. Lakini pia kitabu cha Hesabu 3:14-15 kinasema "Kisha Bwana akanena na Musa huko katika bara ya Sinai, na kumwambia, Uwahesabu wana wa Lawi kwa kuandama nyumba za baba zao na jamaa zao; kila mtu mume tangu umri wa mwezi mmoja na zaidi utawahesabu."

Maandiko yanayoeleza juu ya kuhesabiwa kwa wana wa Israel ni mengi na unaweza kuyasoma baadae ktk (Kutoka 12:37, Waamuzi 20:14, 1 Samweli 11:8, Ezra 2:64).
Kwa hiyo kuhesabiwa ni agizo la Mungu na utamaduni huu wa wana wa Israel kurudi kwao kwenda kuhesabiwa ni utamaduni uliokua maagizo ya Mungu mwenyewe (Jehovah).
Sasa je ikiwa Wachagga hawaendi kuhesabiwa iweje wafananishwe na WaIsrael?
Sababu mbili hufanya wachagga kufananishwa na utamaduni huu wa Israel wa kuhesabiwa.
SABABU YA KWANZA ni kitendo cha wachagga kurudi kwao mwishoni mwa mwaka (December) na kukaa huko hadi mwanzoni mwa mwaka mpya (January). Ikumbukwe wana wa Israel nao huenda kwao mwishoni mwa mwaka wa Kiyahudi (Adar Beit) na kurejea mwanzoni mwa mwaka mpya (Nissan). Ufanano huu wa majira hufanya wachagga nao waonekane kuwa wanaenda "kuhesabiwa" kama waIsrael.

SABABU YA PILI ni mtawanyiko wa jamii hizi mbili. Wana wa Israel wametawanyika ktk mataifa mbalimbali duniani. Kutokana na ufinyu wa nchi yao wamejikuta wakisambaa nchi mbalimbali ambapo wanaishi na kufanya kazi huko. Wengine ni wahandisi, madaktari, majemadari wa vita etc. Wana wa Israel wametawanyika mataifa yote ya Ulaya, America na baadhi ya nchi za Asia na Afrika. Pamoja na kutawanyika huku lakini mwisho wa mwaka hukumbuka kurudi kwao.
Kwa upande wa wachagga nao wametawanyika sana ktk mikoa mbalimbali nchini. Mtawanyiko wao unafananishwa na ule wa wana wa Israel kwa sababu mbili. Kwanza eneo lao la makazi (Kilimanjaro) ni dogo na haliwatoshi, sawa na Israel ilivyo ndogo na isivyotosha watu wake. Pili ni "nature" ya mtawanyiko wao. Wachagga kama Waisrael wametawanyika sehemu mbalimbali za nchi na hata nje ya nchi.

Hakuna mkoa au Wilaya yeyote unaweza kwenda nchini ukamkosa Mchagga. Wametapakaa kila kona ya nchi wakifanya shughuli mbalimbali hususani biashara. Mtu mmoja aliwahi kutania kuwa "ukienda eneo la nchi hii ukakosa Mchagga ondoka haraka maana hapafai kuishi".. Hii ina maanisha Wachagga wanaweza kuishi ktk mazingira yoyote na hali yoyote.

Mtawanyiko wa Wachagga ktk maeneo mbalimbali ya nchi hufananishwa na mtawanyiko wa Waisrael ktk maeneo mbalimbali ya dunia, na hivyo basi kitendo cha Wachagga kurudi kwao mwishoni mwa mwaka hufananishwa na kitendo cha Waisrael kurudi kwao mwishoni mwa mwaka wa kalenda ya kiyahudi. Tofauti ni kuwa Waisrael huenda kuhesabiwa lakini Wachagga hawaendi kuhesabiwa.
KAMA WACHAGGA HAWAHESABIWI, WANAENDA KUFANYA NINI?
Pengine hili ndio swali la msingi ambalo wengi wanajiuliza. Ikiwa wachagga hawaendi kuhesabiwa kama ilivyo kwa waisrael, Je wanaenda kufanya nini?

Ukweli ni kwamba Wachagga wanakwenda kwao kwa sababu mbalimbali. Leo nitaainisha kwa uchache sababu 10 zinazorudisha wachagga kwao kila mwisho wa mwaka. Zipo nyingi zaidi ila kwa kifupi ni kama ifuatavyo;
1. Kuna wanaokwenda kwao kwa ajili ya kuonana na familia zao na kuwaona wapendwa wao na kujumuika nao kwa ajili ya kufurahia sikukuu za mwisho wa Mwaka huhusani "Krismasi" na "Mwaka mpya".

Kwa mfano wazazi wako (baba na mama) au ndugu zako wengine (babu, bibi, kaka, dada, shangazi, wajomba etc) hujawaona kwa kipindi cha mwaka mzima. Mmekuwa mkiwasiliana tu kwa simu. Hivyo basi December huwa ni kipindi kizuri cha kurudi nyumbani na kuwaona na kuwajulia hali.

2. Pia kipindi hiki hutumika kupanga mipango ya maendeleo ya familia kama vile kujenga. Kwa kuwa watoto wote wa familia hukutana kipindi hiki basi huweka mipango ya maendeleo kwa familia yao. Wanaweza kupanga kujenga nyumba kwa ajili ya wazazi wao ambao ni wazee, kuweka umeme, maji etc.
Uchaggani ni mojawapo ya maeneo nchini ambako kuna nyumba nyingi za kisasa vijijini na ni mkoa uliofanikiwa kupiga vita nyumba ya Nyasi tangu mwaka 1996.
Ni jambo la Kawaida kukutana na maghorofa ya kisasa kule "Machame Uswaa, Kibosho Kirima, au Mamba Komakundi".. au ukipita "Uru Mawela, Rombo Mamsera au Kilema Poffo" nyumba zote unazokutana nazo ni self-contzined za kisasa, lakini wanaishi wazee. Watoto wao wapo Shinyanga, Dar, Kigoma, Mwanza etc wanatafuta maisha. Mipango hiyo ya kujenga na kuhudumia wazazi hupangwa msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

3. Msimu huu wa sikukuu hutumika kupatanisha ndugu, jamaa au marafiki waliokosana. Wazee huitwa na kuzungumza na pande zote mbili kisha kuwapatanisha. Mkikubali kuelewana basi huchinjwa mbuzi kama ishara ya furaha ambapo jamii yote hujumuika kwa kula na kunywa.

4. Kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ndio kipindi kizuri ambacho vijana hukitumia kutambulisha wachumba zao nyumbani. Unaweza kuwa unaishi Dar na umepata mchumba wa Morogoro. Lakini ndugu zako wametawanyika. Wengine wapo Tabora, wengine Mwanza, wengine Mbeya. Huwezi kupita na mchumba wako kote huko kumtambulisha. Kwahiyo "option" nzuri ni kusubiri msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka ambapo ndugu zako wote watakuwepo nyumbani ndipo umpeleke mchumba wako kumtambulisha, na kupanga mipango ya ndoa.

5. Kuwaleta watoto wafahamu ndugu zao na wafahamike nyumbani. Unaweza kuwa unaishi Dar na familia lakini ndugu zako wanaishi na familia zao maeneo mengine ya nchi, watoto wenu hawafahamiani maana hawajawahi kuonana. Hivyo mkikutana nyumbani msimu wa sikukuu ni kipindi kizuri cha watoto wenu kufahamiana na kufahamu asili yao.
Pia ikiwa umejaliwa mtoto ukiwa huko unakofanyia shughuli zako lakini wazazi wako hawajamuona mjukuu wao, hiki ni kipindi kizuri cha kuwapelekea wazazi wako mjukuu wao wamuone na kumpa baraka.

6. Kushiriki shughuli za kijamii (charity work). Wachagga wengi ni waumini wazuri sana wa dini iwe ukristo au uislamu. Hivyo kipindi cha msimu wa sikukuu hutenga muda wa kutembelea wagonjwa, Yatima na Wasiojiweza na kuwapa misaada mbalimbali. Kwa wale Wakristo huita "sadaka ya Epifania".

7. Kipindi hiki hutumika pia kufanya usafi na kurekebisha maeneo waliyopumzika wapendwa wetu (makaburi). Wachagga kama ilivyo binadamu wengine hutenga maeneo maalumu ya kuzikia ndugu zao; na mara nyingi kila familia ina eneo lake.

Kwa hiyo ikiwa kuna ndugu amefariki na akazikwa basi msimu huu huwa ni kipindi kizuri cha kujengea makaburi kama kumbukumbu ya sehemu walipopumzika wenzetu.
Bahati mbaya wapo watu wanaohusisha utamaduni huu na matambiko. Kwanza ieleweke kujengea makaburi si dhambi na si matambiko. Hata Yakobo alipofia kule Misri alipoenda kwa mwanae Yusufu alizikwa kwenye Kaburi lililojengewa (Matendo 7:15-16). Hivyo basi ni vizuri ikaeleweka kuwa kujengea makaburi si dhambi.

Na mara nyingi uchaggani kabla ya kujengea Kaburi kiongozi wa dini huitwa na kufanya sala, kabla ya shughuli ya ujenzi haijaanza. Kwahiyo hakuna nafasi ya matambiko.
Ikiwa kuna mchagga anafanya matambiko wakati wa kujengea makaburi ichukuliwe kuwa ni tabia ya mtu binafsi na isihuhishwe wachagga wote. Kwani wapo watu wa makabila mengine hufanya matambiko pia lakini huwezi kusema jamii yote hutambika.
8. Msimu huu wa sikukuu ni kipindi kizuri ambacho wachagga hukitumia kupanga na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ya jamii yao kama vile mashule, hospitali, Maji, barabara n.k
Kwa mfano zipo barabara nyingi ambazo zimejengwa kwa nguvu ya wananchi wenyewe kwa kuamua kujichangisha bila kusubiri serikali ifanye. Barabara ya Uru Kusini ni mojawapo. Mipango hii hupangwa msimu huu wa sikukuu.

9. Msimu huu hutumika kwa ajili ya mapumziko ya familia baada ya mahangaiko ya mwaka mzima. Ni wakati wa familia kutulia pamoja kutafakari mipango ya mwaka uliopita na kuweka mipango mipya ya mwaka unaofuata.
Ndugu na jamaa hukutana pamoja na kufurahia sikukuu za "Krismasi" na "mwaka mpya" kwa kula na kunywa hasa vyakula vya asili kama "kisusio, faya, supu ya mbuzi iliyopikwa kiasili kwa kuchanganywa na majani aina ya "mahombo" na vyakula vingine bila kusahau kinywaji aina ya mbege.

10. Kipindi hiki hutumiwa kujenga na kukarabati nyumba za ibada. Ni wazi kuwa Kilimanjaro ni miongoni mwa maeneo ambayo kuna nyumba nzuri na za kisasa za Ibada.
Kanisa kubwa na la kisasa kama la KKKT Old-Moshi Rau, au La RC Kristu Mfalme, Au TAG Kilimanjaro Revival, au Msikiti wa kisasa kama wa Riadha, ni nadra kuvipata mahali pengine. Au Kanisa la kale kama la KKKT Old-Moshi Kidia lililojengwa mwaka 1843 utalipata wapi kwingine?
Mipango ya ujenzi wa nyumba hizi za ibada za kisasa na kukarabati zile za zamani hufanywa msimu huu wa sikukuu.

Pia wachagga wengi hupenda kwenda kwao kwa kuwa ibada zote ktk msimu huu huongozwa kwa kichagga. Yani kuanzia usomaji wa misa, mahubiri hadi nyimbo huimbwa kwa kichagga, wakati huo nyumba za ibada zimepambwa kwa mapambo ya asili kama "Makurera, makangachi, migomba imechimbiwa vichumini (njia za kwenda nyumbani)" etc.

Hii huongeza nakshi na kufanya mtu ajisikie kupungukiwa kitu ikiwa hatakuwepo Nyumbani msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

NB: Utamaduni huu wa Wachagga ni mzuri sana, na kuna mengi jamii nyingine zinaweza kujifunza kupitia Wachagga kama ambavyo wachagga wanaweza kujifunza kupitia jamii nyingine.
Tuukatae uzungu, tujivunie vya kwetu. Jivunie usukuma wako, jivunie Usambaa wako, jivunie Unyakyusa wako, jivunie Umasai wako, Jivunie Ungoni wako, najivunia Uchagga wangu. SI KOSA kujivunia kabila lako lakini NI KOSA kutumia kabila lako kumbagua mtu wa kabila jingine.

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UAGIZAJI WA NYAMA YA KUKU KUTOKA NJE YA NCHI

Serikali imepiga marufuku kuagiza na kuingiza nyama za kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi ili kulinda afya za walaji wa bidhaa hiyo ya nyama nchini.
Katazo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mhe. William Tate Ole Nasha kwenye mahojiano maalum na EATV ilipotaka kupata ufafanuzi wa serikali kuwa inahakikisha vipi nyama na vitoweo kutoka nje ya nchi zinaingizwa nchini zikiwa na ubora unaokidhi viwango vya afya kwa walaji.Ole Nasha amesema hairuhusiwi kuagiza wala kuuza kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi kwakuwa kwa sasa nchi inajitosheleza na inajitegemea kwa kiwango kikubwa cha nyama.
Amewataka wafugaji na wafanyabiashara kutumia fursa za kuzalisha nyama kwa tija na ubora zaidi ili nchi ianze kuuza vitoweo vya nyama hasa kuku nje ya nchi.
Ameongeza kuwa tayari serikali inaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa viongozi wanaoshirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kuingiza nyama hizo za kuku wa nje nchini

Friday 23 December 2016

VITUKO: ZAWADI YA XMAS

XMAS NA USAFIRI

Kipindi hiki kuelekea sikukuu za xmas na mwaka mpya, kituo cha Mabasi Ubungo kimekuwa kikizidiwa wingi wa abiria kiasi cha kujikuta, daladala nazo zalazimika kusafirisha abiria wa mikoani

Thursday 22 December 2016

Wednesday 21 December 2016

UJUE MGAHAWA WA STAA SHILOLE "Shishi"

Yapata Mwezi sasa umepita tangia Shilole afungue Mgahawa wake na tayari matunda yana onekana kwani mrembo huyo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio amesema anaingiza faida ya Laki Tano Tsh 500,000/= kwa siku.
“Mimi hata kama waniite mama ntilie ila najua mwisho wa siku naingiza mkwanja wangu sipungukiwi kitu nauza chakula na jioni naingiza laki tano wewe endelea tu kupiga majungu mimi napiga kazi“Amesema Shilole

Monday 19 December 2016

MHE RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MMOJAWAPO NI MKUU MPYA WA WILAYA YA UBUNGO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 2 na Wakurugenzi 3 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Kisare M. Makori kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Bw. Kisare M. Makori anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Humphrey Polepole ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi.

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Avod Mmanda Herman kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara iliyopo katika Mkoa wa Mtwara.

Bw. Avod Mmanda Herman anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Khatib M. Kazungu ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga iliyopo Mkoani Shinyanga.

Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Lewis Kalinjuna ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw Rojas John Romuli kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda iliyopo katika Mkoa wa Katavi.

Bw. Rojas John Romuli anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ngalinda Hawamu Ahmada aliyefariki dunia hivi karibuni.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Rashid K. Gembe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Bw. Rashid K. Gembe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Mkumbo Emmanuel Barnabas ambaye uteuzi wake ulitenguliwa hivi karibuni.

Uteuzi wa huu unaanza mara moja na wateule wote wanatakiwa kuripoti Makao Makuu ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) mara wapatapo taarifa hii.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

19 Desemba, 2016

Sunday 18 December 2016

Saturday 17 December 2016

Thursday 15 December 2016

LOWASSA: "JPM ACHANA NA KUNUNUA NDEGE"

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa, ametaka vijana wa chama hicho kukabiliana na ukandamizaji wa demokrasia aliodai unafanywa na watawala.

Alisema hayo juzi alipokutana na vijana wa chama hicho ambao ni wanavyuo (CHASO) wa vyuo vikuu mkoani hapa.

Lowassa ambaye yuko Tabora kwa ziara ya kuimarisha chama, aliwataka vijana hao kuwa na ujasiri wa kukabiliana na ukandamizaji wa demokrasia kwani vijana duniani ndio chachu ya mabadiliko.

“Nimekuja Tabora kuwashukuru kwa kura nyingi mlizonipigia na hamasa kubwa mliyoionesha kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Katika uchaguzi ule tulishinda, lakini ushindi mkubwa zaidi ni tulipofanikiwa kuvumilia na kuweka maslahi ya watoto, wazee na mama zetu mbele," alisema na kuongeza:

"Amani ni tunu muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa kuliko kitu kingine chochote. Msikate tamaa, tumejipanga vema kwa uchaguzi ujao wa mwaka 2020 na hatutadhulumiwa tena haki yetu, kama ilivyokuwa mwaka jana,” alisema Lowassa.

Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani, alisema Jambo Kuu na la msingi ambalo wana Chadema wanatakiwa kuwa nalo sasa katika chama ni umoja na mshikamano kati yao.

"Umuhimu wa umoja na mshikamano ndani ya chama chetu ni mkubwa sana, hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali inajaribu kwa kila namna kukandamiza Upinzani na demokrasia na jambo hili si geni, ukirudi nyuma katika historia ya vyama vya siasa nchini, hata kabla ya Uhuru, unaweza kuona umoja ulivyoisadia TANU dhidi ya chokochoko za chama alichoanzisha mkoloni wakati ule - United Tanganyika Party (UTP) kukabiliana na kuidhoofisha TANU na kumzuia Mwafrika kupata Uhuru na kujitawala," alisema.

Aliwaambia vijana kwamba changamoto kama hizo ni za kawaida kwa vyama vingi vya upinzani hasa Afrika, ambavyo vinaungwa mkono na wananchi wengi wakiamini ni vya ukombozi.

Lakini pia alisema katika kujenga umoja na mshikamano huo ndani ya chama, ni lazima nguvu kubwa ipelekwe kwenye matawi waliko wananchi.

"Katika chama chochote cha siasa watu wengi hawako ngazi za juu, bali mashinani. Ni lazima nguvu yetu kubwa ielekezwe huko kwa sasa, ili kuhakikisha chama kinakuwa na misingi madhubuti ambayo inaweza kutumika kukisaidia nyakati za uchaguzi," alisema.

Aidha, Lowassa ambaye katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana alipata asilimia 38 ya kura, alihoji umuhimu wa Serikali kununua ndege zaidi, kuliko kupeleka huduma muhimu vijijini.

"Tumesikia nia njema yao ya kuagiza ndege nyingine zaidi miaka miwili ijayo, lakini tunajiuliza, je isingekuwa busara kutumia fedha hizo kupeleka maji safi na salama mijini na vijijini?" Alihoji.

Wednesday 14 December 2016

MZEE WA UPAKO

Siku moja baada ya Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo maarufu Mzee wa Upako kusema waandishi waliomuandika vibaya watakufa kabla ya Machi 2017, Jeshi la Polisi linatarajia kutoa msimamo wake dhidi ya kauli hiyo leo.

Kauli hiyo ya Mzee wa Upako aliyoitoa juzi kanisani kwake, ilikuwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo akijibu yale yaliyoandikwa katika vyombo vya habari kuhusu madai ya kulewa na kumfanyia fujo jirani.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Kipolisi ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro jana alisema ni mapema kuzungumzia sakata hilo kwa sababu jana ilikuwa sikukuu na atatolea ufafanuzi leo.

“Anasema hao waandishi watakufa kabla ya Machi 2017 kwani yeye Mungu? Hilo ni suala zito, tumeandaa mkutano na waandishi wa habari tutalizungumzia suala hilo kesho (leo),” alisema Kamanda Sirro.

Katika kauli hiyo, Mzee wa Upako alisema kila mwandishi aliyemuandika vibaya ikifika Machi mwakani hatakuwa hai na kama wataendelea kuishi, ataacha kazi ya kuhubiri injili na kwenda kuuza gongo.
Pamoja na Kusulubiwa na Wayahudi na hata kufia Msalabani lakini bado YESU alimwambia MUNGU "Baba wasamehe watu hawa"
Sasa Mzee wa Upako kuandikwa Kalewa tu tayari anasema "Waandishi hamfiki Mwezi wa tatu mnakufa...Baba waue la sivyo naenda kuuza Gongo"😂😂😂😂😂😂
Huyu Mtumishi wa Mungu sijui anatumia agano la Kati,maana Agano la Kale na Jipya hivi vitu vya kisasi havimo

Tuesday 13 December 2016

HUMPHREY POLEPOLE ATEULIWA KUWA KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI CCM

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Humphrey Polepole alieteuliwa kuwa Katibu Uenezi CCM
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Makamu Mwenyekiti wa (CCM Zanzibar) Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Philip Mangula kabla ya kuanza kikao cha CCM kufanya uteuzi wa wajumbe mbalimbali jijini Dar es Salaam

Monday 12 December 2016

HERI KWA SIKUKUU YA MAULID

Katika kusherekea siku ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammed (S.A.W), Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuwatumikia Watanzania wote bila kujali imani zao za kidini. Majaliwa ameyasema hayo katika sherehe za kitaifa za Maulid ambazo zimefanyika mkoani Singida

Sunday 11 December 2016

JE WAZIJUA AU WAZIKUMBUKA SARAFU HIZI ZA TANZANIA?

MELI YENYE MALORI 600 YA DANGOTE YAWASILI MTWARA


Mfanyabiashara Alhaji Aliko Dangote jana alipokuwatana na kufanya mazungumzo na Rais Dk Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam alimthibitishia kuwa hana lengo la kufunga kiwanda chake kama inavyodaiwa badala yake anatafuta fursa nyingine za kuwekeza hapa nchini; Alitamka kuleta malori 600 kwa ajili ya usambazaji wa DANGOTE CEMENT na hii ni fursa ya ajira kwa madreva 600

Katika kuthibitisha hilo, Mfanyabiashara huyo alisema leo meli yenye malori mapya 600 kwa ajili ya kusambazia saruji yake itawasili nchini. Ameongeza kuwa lengo la kufanyabiashara hapa nchini mbali na kutengeneza faida pia ana lengo la kuisaidia serikali ya Tanzania kutengeneza ajira hivyo hana sababu ya kuagiza mali ghafi toka nje ya nchi ambazo zinapatikana nchini.

Baada ya kufanya mazungumzo hayo, meli yenye magari hayo 600 imetia nanga katika bandari ya Mtwara ambapo ndipo kiwanda cha Saruji cha Dangote kilipo.

Aidha, imeelezwa kuwa wiki ijayo meli nyingine kutoka Korea Kusini yenye malori 451 inatrajiwa kuwasili katika bandari ya mkoani Mtwara.

MAMBO YA MCHINA: TAFADHALI USIIGE!

Saturday 10 December 2016

MFANYABIASHARA DANGOTE WA NIGERIA AFANYA MAZUNGUMZO NA MHE RAIS MAGUFULI

Rais Magufuli amemhakikisha mfanyabiashara wa Nigeria, Aliko Dangote kuwa itamwekea mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuhakikisha kiwanda chake cha saruji kinaendelea kufanya kazi kwa ufanisi.

Rais amesema kuna ‘wapiga deal’ walikuwa wameingilia mradi wake huku Dangote akisema mwezi huu analeta malori 600 kwaajili ya shughuli zake na kubebea saruji na kwamba atanunua kila rasilimali kwaajili ya kiwanda hicho hapa hapa Tanzania. Pia amedai kuwa atatengeneza ajira zingine mpya zaidi ya 1,500.

Thursday 8 December 2016

UJUMBE MUHIMU KUHUSU KUKWEA MLIMA KILIMANJARO

Mlima Kilimanjaro uliopo mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania waonekana pia ukiwa nchini Kenya, ila njia (Routes) za kuukwea ni kupitia Tanzania tu maana ni wa Tanzania

MHE,RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO YA VIONGOZI MBALIMBALI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 07 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Katibu Mkuu mmoja na Mkuu wa Mkoa mmoja na pia amefanya mabadiliko madogo katika Wizara na Mikoa kama ifuatavyo;

Dkt. Magufuli amemteua Prof. Faustin Kamuzora kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais.Kabla ya uteuzi huo, Prof. Kamuzora alikuwa Katibu Mkuu Mawasiliano.

Rais Magufuli amemteua Mhandisi Mathew Mtigumwe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo anayeshughulikia Kilimo. Mhandisi Mathew Mtigumwe anachukua nafasi ya Dkt. Frolence Turuka ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Frolence Turuka alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi aliyekuwa akishughulikia Kilimo. Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Job Masima ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Rais Magufuli amemteua Dkt. Maria Sasabo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na atakuwa akishughulikia Mawasiliano. Dkt. Maria Sasabo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Faustin Kamuzora ambaye ameteuliwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais.

Pia Rais Magufuli amemteua Mhandisi Angelina Madete kuwa Naibu Katibu Mkuu Katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Mhandisi Angelina Madete anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Maria Sasabo aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Mawasiliano.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce K. Nzuki kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Bw. Christopher Ole Sendeka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.Bw. Christopher Ole Sendeka anachukua nafasi ya Dkt. Rehema Nchimbi ambaye amehamishwa kituo cha kazi na kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Dkt. Rehema Nchimbi anajaza nafasi iliyoachwa na Mhandisi Mathew Mtigumwe ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo anayeshughulikia Kilimo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Dkt. Osward J. Mashindano kuwa Msajili wa Hazina.

Dkt. Osward J. Mashindano anachukuwa nafasi ya Bw. Lawrence Mafuru ambaye atapangiwa kazi nyingine

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasilino ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

07 Desemba, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo tarehe 07 Desemba Ikulu jijini Dar es Salaam. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. PICHA NA IKULU

Wednesday 7 December 2016

GOODNEWS: DIAMOND NA ZARI WAPATA MTOTO WA KIUME

Hatimaye Zari na Diamond wamefanikiwa kupata mtoto wa kiume aliyezaliwa saa 10:35 alfajiri kwa saa za Afrika Mashariki, Jumanne, Desemba 6. Mtoto huyo amezaliwa kwenye hospitali ya NETCARE ya Pretoria Nchini Afrika ya Kusini



Sunday 4 December 2016

TAREHE RASMI YA SIKUKUU YA MAULID

MISS AFRICA 2016

Mrembo wa Angola, Neurite Mendes ameibuka mshindi wa mashindano ya Miss Afrika 2016 Jumamosi iliyopita, na hivyo kuwa Balozi wa kwanza wa mabadiliko ya tabia nchi Afrika.

Saturday 3 December 2016

KARIBU UJENZIZONE

Kwa mahitaji yako ya vifaa, ushauri, contact za mafundi ujenzi jiunge na www.ujenzizone.blogspot.com