Thursday 19 June 2014

MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA

Najua huu ni msemo unaotumiwa san ana viongozi wetu, na bahati mbaya ni pale wanapoomba kura. Lakini tunawakumbusha kuwa wajitahidi kutekeleze ahadi zao maana kwakweli hali za walio wengi zinatisha. 
Hatukatai viongozi kutembelea Land Cruiser V8 za mamilioni ya fedha, lakini mwaona hawa waliowapigia kura wana makazi gani na huo usafiri wao hapo nje???

Tungefurahi huduma za afya kusogezwa karibu na wananchi na sio kuwaza kupeleka wagonjwa kutibiwa nje ya nchi. Katika mazingira haya kweli huyu mgonjwa ataona ahueni yoyote?

Haya nayo ni makazi, mvua zikinyesha je?

Mzalendo wa kweli.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako