Friday 27 June 2014

HII HAIKUBALIKI

Imekuwa tabia inayozoeleka kwa Matrafiki kujificha sehemu na kisha kutokea barabarani ghafla na kusimamisha gari kwa lengo la kukagua makosa. Ni sawa kwamba ukaguzi wa magari kuhakikisha usalama ni muhimu, lakini kwa staili hii ni mbaya maana wakati mwingine dreva anapata mshtuko na yaweza kusababisha ajali. Ni vema Maafisa hawa wakawa wanatumia utaratibu unaoeleweka. Hata hivyo ni muhimu pia kwa madreva na wamiliki wa vyombo vya moto kujitahidi kufuata sheria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vyombo vyao ni salama kwa usafiri wa abiria na mali zao.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako