Friday 10 April 2015

ZA MWIZI AROBAINI: ALAZIMISHWA KULA MAHINDI MABICHI

Jamaa ambaye jina halikuweza kupatikana mara moja, amejikuta akionja joto ya jiwe baada ya kudaiwa kukutwa akiiba kwenye shamba la mahindi hivyo kulazimishwa kula mahindi mabichi.Tukio hilo la aina yake lilijiri hivi karibuni kwenye Kata ya Miembeni, Bukoba mkoani Kagera na kuibua gumzo kubwa.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, baada ya kumnasa kijana huyo akiiba mahindi aliyoyajaza kwenye gunia, wamiliki wa shamba hilo walimuamuru kukaa chini na kuyala yakiwa mabichi hadi yaishe, kitendo ambacho jamaa huyo alikubaliana nacho.
(Picha na maelezo kwa hisani ya Le Mutuz)

2 comments:

Maoni yako