Wednesday 22 April 2015

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU: MNAOWANIA UONGOZI JIANDAENI KUTULETEA UWIANO WA HUDUMA MUHIMU NA MAENDELEO ZAIDI

1. MICHEZO YA WATOTO
Watoto wanahitaji maeneo ya kuchezea. Sehemu nyingi zilizokuwa wazi zimetengwa kwa ajili hiyo zimeingilia na kutumika vinginevyo.
Wakati hao wa mazingira magumu wanacheza peku kwenye mawe, wengine waliojaaliwa wanafurahia mazingira mazuri.
2. USAFIRI
Hili nimekuwa tatizo kila kukicha. Mfano kwa Jiji la Dar, msongamano wa magari na usafiri kutokidhi kunawapa watu wengi adha. Hali hii imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo sana.
Lakini hatuachi kushukuru kwa juhudi za serikali kuboresha hili.
3. MAKAZI
Bado wananchi wengi wanaishi katika mazingira magumu kimakazi. Tunaomba hili litupiwe macho
Hata hivyo juhudi za serikali na watu binafsi kuboresha maisha zinaonekana. Ni bidii iongezwe tu
4. MAJI
Wananchi wanateseka kwa adha hii
Hata hivyo juhudi katika baadhi ya maeneo zimefanyika na wananchi wanapata maji safi na salama. Ila sio wote. Tanzania ilivyojaliwa mito na maziwa inawezekana tatizo la maji likawa historia

2 comments:

Maoni yako