Monday 20 April 2015

WAZIRI MEMBE: HAKUNA MTANZANIA ALIYEFARIKI KATIKA MAPIGANO AFRIKA KUSINI

Watanzania 23 waishio Afrika Kusini wamewekwa kwenye kambi maalumu ya Isipingo nchini humo ili kupewa ulinzi wa maisha yao yaliyo hatarini kufuatia mashambulizi yanayofanywa na wazawa dhidi ya wageni.

Watu hao ambao ndiyo idadi ya Watanzania waliotambulika kuwa hatarini nchini humo, wanatarajia kuwasili nchini muda wowote baada ya Serikali ya Afrika Kusini kuridhia.

Watakaorejea nchini ni Watanzania 21, wengine wawili wameomba kuendelea kubaki huko.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema hakuna Mtanzania aliyepoteza maisha katika vurugu zilizosababishwa na chuki dhidi ya wageni, lakini wapo Watanzania watatu waliokufa nchini humo kwa sababu nyinginezo

Goodwill Zwelithini, Mfalame wa Zulu ambae inasemekana matamshi yake ndo yalopelekea mapigano haya huko Africa Kusini, japo leo kajitokeza akiwaasa wananchi hao waache fujo

No comments:

Post a Comment

Maoni yako