Friday 3 April 2015

IJUMAA KUU

Wakristo pote duniani leo wameungana kukumbuka mateso na kifo cha Yesu anayekadiriwa kufa tar 7 April 30 nje kidogo ya Mji wa Jerusalem. Ibada mbalimbali za kukumbuka mateso na kifo chake yamefanyika katika makanisa mbalimbali majira ya alasiri. Hii ni mojawapo ya siku muhimu kuelekea sikukuu ya Pasaka hapo Jumapili
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akiubusu msalaba wakati wa Ibada Takatifu ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mt.Yosef Jijini Dar es Salaam.

Waumini wakifuatilia ibada ya Ijumaa kuu katika kanisa la KKKT Azania Front Dar

Igizo la mateso ya Yesu

No comments:

Post a Comment

Maoni yako