Sunday 22 March 2015

MGOGORO WA MAGARI YA KITALII NA SAFARI ZA NDEGE KATI YA KENYA NA TANZANIA WATATULIWA

Imekubaliwa sasa kuwa ni ruksa magari ya kubeba watalii kutoka Tanzania kuingia katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta, ambapo hapo awali walizuiwa. Pia safari za Ndege la Shirika la ndege la Kenya Airways zimerudishwa kama mwanzo 42 kwa wiki. Makubaliano haya yamefikiwa na Maraisi wa nchi hizi mbili katika kikao cha dharura walichofanya huko Windhoek Namibia walipoenda kuhudhuria sherehe za miaka 25 ya Uhuru na pia kuapishwa Rais mpya wa 3 wa nchi hiyo.
Maraisi Mhe Uhuru Kenyatta (Kenya) na Mhe.Jakaya Kikwete (Tanzania) wakiwa katika kikao cha dharura kutatua mgogoro huu huko katika Hotel ya Safari Court jijini Windhoek,Namibia.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako