Monday 23 March 2015

KUMBUKUMBU

Mmiliki wa Blog hii anaungana na familia na Ukoo wa Mwangoka kumkumbuka Baba Mzazi Mzee Amedeus Mwangoka aliyetutoka tar.23.03.2009 siku ya Jumatatu kama leo katika Hospitali ya Kibosho-Moshi. Tulikupenda sana Baba na kamwe hatutasahau busara zako na uchapakazi wako makini kutuwezesha wanao kuishi,kusoma na kukua kiroho na kimwili. Pengo lako kamwe halitazibika. Tunakuahidi kukuenzi kwa kuishi tunu zako. Tunakuombea Mungu akupumzishe palipo pema mbinguni. Tutakukumbuka daima Baba yetu. "Bwana alitoa na Bwana ametwaa,Jina la Bwana lihimidiwe" Amen.
Mzee Amedeus Mwangoka enzi za uhai wake huko nyumbani kwake Sanya Juu-Kilimanjaro
Taswira ya Mwana Karibu Nyumbani (Mtoto wa tatu wa marehemu) siku ya mazishi

2 comments:

Maoni yako