Sunday 17 May 2015

RAIS WA ZAMANI WA MISRI MORSI AHUKUMIWA KIFO

Mahakama nchini Misri imemuhukumu adhabu ya kifo aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo Mohammed Morsi kwa kosa la kuchochea machafuko wakati wa maandamano Desemba mwaka 2012 yaliyolenga kupinga uongozi wake.

Mohammed Morsi alikutwa na hatia hiyo baada ya kukamatwa waandamanaji waliokuwa wakipinga serikali yake, hivyo jeshi kumtimua madarakani Julai 2013.

Mohamed Morsi alishirikishwa katika kesi hiyo pamoja na viongozi na wafuasi wengine 12 wa Kundi la Kiislam Muslim Brothehood, ambao mwanzoni (mwezi uliopita) walihukumiwa pia kifungo cha miaka 20 jela.

Morsi ndiye aliyekuwa kiongozi wa kwanza (rais) aliyechaguliwa kwa njia kidemokrasia nchini Misri licha ya kuhukumiwa kifo.
Waendesha mashtaka wanamtuhumu Mohamed Morsi na viongozi wengine wa Muslim Brotherhood kuchochoea machafuko yaliyosababisha mamia ya waandamanaji nchini Misri kufariki dunia Desemba mwaka 2012.

Hisia tofauti zimetolea nchini Misri baada ya uamzi huo wa Mahakama kutangazwa na jaji mmoja wa mahakama ya nchi hiyo, Shaaban el-Shami.

Raia wanaomuunga mkono Mohamedi Morsi wamepokea kwa shingo upande uamzi huo. Wengi walidhani kwamba rais huyo wa zamani wa Misri angepunguziwa adhabu yake ya mwanzo ya kifungo cha miaka 20 jela.

Kwa upande wao raia wasiomuunga mkono wamenukuliwa wakisema kuwa hukumu aliyopewa inafaa ikilinganishwa vitendo alivyovifanya wakati akiwa madarakani.

Kwa upande wao, wafuasi wa Muslim Brotherhood ambao wamezungumza na vyombo vya habari vya kigeni na vile vinavyopeperusha kwenye mitandao mbalimbali, wamebaini kwamba kesi hiyo ni ya kisiasa, ambayo imekua ikiandaliwa na kundi la wanajeshi waliohusika katika kuupindua utawala wa Morsi.
CHANZO: NA IRAN SWAHILI
Machafuko yaliyotokea nchini Misri.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako