Saturday 9 May 2015

BASI LA DAR EXPRESS LAWAKA MOTO LIKIWA SAFARINI

Linahesabika kama tukio jingine la Basi kuwaka moto katika rekodi za mabasi yaliyowaka moto yakiwa safarini nchini Tanzania wakati yakiwa na abiria.
Taarifa zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi Pwani SACP Jafari Ibrahimu baada ya kuongea ni kwamba basi hili la kampuni ya Dar Express liliwaka moto likiwa safarini kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha likiwa limejaa abiria

Basi hilo mali ya Kampuni ya Dar Express lenye namba za usajili T833 DDR likiwaka moto na kuteketea kabisa hii leo majira ya saa 7:30 mchana katika kijiji cha Kwamakocho,Kata ya Mandera, Tarafa ya Miono, Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako