Tuesday 30 August 2016

NDEGE ZILIZONUNULIWA NA TANZANIA HUKO CANADA KUWASILI NCHINI MUDA WOWOTE SEPTEMBA

Hii ndio moja ya ndege mpya ya Air Tanzania iliyo tayari kwa kila kitu.Hapa ipo kwenye Hangar(eneo la matengenezo ya ndege) nchini Canada tayari kwa kuanza safari ya kuja Tanzania.Wakati wowote na siku itakayotajwa ya mwanzoni mwa mwezi September ndege hizi mbili zitatuwa katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dsm.
Hakika ndege hizi ni rafiki kwa mazingira ya viwanja vya Tanzania na usafiri wa ndani.Itasaidia kutua hata katika viwanja "korofi" kama Mtwara,Kigoma,Tabora,Iringa,Songea,Dodoma(japo nasikia inafanyiwa ukarabati) na viwanja vingine kama Arusha,Mwanza,Znz,Tanga na Mbeya.
WELCOME TO THE MARKET ATCL.....THE WINGS OF THE KILIMANJARO

No comments:

Post a Comment

Maoni yako