Tuesday 30 August 2016

MHE AUGUSTINE MREMA AWAOMBEA KAZI MATEJA

Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Palore nchini, Dkt. Augustino Lyatonga Mrema, amemwomba Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuongeza maeneo ya kutoa tiba ya kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.

Sambamba hilo, Mrema amemuomba Rais kuwasaidia wahanga wa dawa za kulevya waliopatiwa tiba kurejea katika shuguli za kuzalisha uchumi.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo wahanga wa dawa za kulevya nchini, Dkt. Mrema amelitaka jeshi la polisi kuacha mara moja kuwanyanyasa waathirika wa madawa hayo huku akimtaka Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwapatia ajira pindi wanapoacha kutumia madawa hayo.

Naye Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili kutoka Hosptali ya Taifa Muhimbili Kitengo cha Madawa ya Kulevya Dkt. Cassian Nyandindi amesema ni vyema serikali ikajenga maeneo mengine nchini ya kutoa huduma ya matibabu kwani maeneo matano pekee yaliyopo nchini hayatoshi kuweza kuwahudumia waathirika hao ambao wanaongezeka kila siku.

EATV ilifanya mahojiano na baadhi ya waathirika wa dawa za kulevya ambao wamelilalamikia jeshi la polisi kuchukua fedha zao huku kila mara wakiwahusisha na kuuza dawa za kulevya ambazo tayari wameacha kutumia.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako