Wednesday 17 February 2016

UGANDA: MHE RAIS MUSEVENI AWANIA AWAMU YA TANO MFULULIZO

Rais Yoweri Museveni aliwahi kusema kuwa viongozi wanaokaa sana madarakani ndiyo walikuwa chimbuko la matatizo ya Afrika, lakini miaka 30 baadae, Museveni anatazamia kuingia muongo wa nne madarakani nchini Uganda.
"Wale wanaosema, 'aende,' wanahitaji kufahamu kuwa huu siyo wakati sahihi," Museveni alisema wakati wa mmoja ya mikutano yake ya kampeni hivi karibuni kuelekea uchaguzi mkuu wa Februari 18 ambao wengi wanataraji atashinda. "Mzee huyu ameiokoa nchi hii, vipi unamtaka aondoke? Ninaweza kuondoka kwenye shamba la migomba niliopanda na ambayo imeshaanza kuzaa matunda?"
Museveni alifanikiwa kubadilisha katiba mwaka 2005, na kuondoa ukomo wa mihula miwili. Viongozi wengine wa Afrika wamefuata nyayo zake, wakibadili au kurekebisha sheria ili kusalia madarakani, wa karibuni zaidi wakiwa marais wa Burundi Pierre Nkurunziza na wa Rwanda Paul Kagame.
Kwa sasa, Museveni hana nia ya kukabidhishi madaraka kwa mtu yeyote, akipinga ukosoaji wa mataifa wahisani ya magharibi kuhusiana na kukithiri kwa rushwa na hatua za kutoa madaraka makubwa kudhibiti mashirika ya kiraia na yale yasiyo ya kiserikali.
Wakati akiwania kuingia muongo wake wa nne madarakani, Museveni anaednelea kuwa mmoja wa viongozi wajanja na ving'ang'anizi zaidi barani Afrika, sambamba na wengine mifano ya Jose Eduardo dos Santos wa Angola na Teodoro Obiang wa Guinea ya Ikweta (wote wako madarakani tangu 1979), Robert Mugabe wa Zimbabwe (tangu 1989) na Paul Biya wa Cameron (tangu 1982).
Kwa sehemu kubwa, Uganda imekuwa na amani wakati wa utawala wa Museveni. Uasi wa kaskazini, unaoongozwa na kichaa wa miujiza Joseph Kony na kundi lake la Lord's Resistance Army (LRA), ulifurushwa nje ya nchi hiyo muongo mmoja uliyopita na mkono wake imara umezuwia machafuko ya kutumia silaha na ugaidi.
Hali ya uchumi iliboreka na Uganda ilishuhudia ukuaji wa asilimia 7 katika miaka ya 1990 na 2000, ukisukumwa na uwekezaji wa umma katika miundombinu na kufufuka kwa kilimo. Pia aliendesha kampeni yenye ufanisi dhidi ya maradhi ya ukimwi na maambukizi yake.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako