Wednesday 17 February 2016

FIRST LADY MAMA JANETH MAGUFULI ATEMBELEA SHULE YA MBUYUNI KUWASALIMU NA KUWAAGA RASMI


LEO Feb 17 2016, Mke wa Rais John Pombe Magufuli Janeth Magufuli amewasili katika shule ya msingi Mbuyuni, Dar kwa ajili ya kuagana na walimu wenzake pamoja na wanafunzi aliokuwa akiwafundisha

Shule ya Msingi Mbuyuni ni shule ambayo Mama Magufuli alisoma kuanzia darasa la kwanza na baadaye mwaka 1995 kurudi tena kufundisha hapohapo kwa miaka 17 hadi mumewe Rais Magufuli alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanzania.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea zawadi ya saa toka kwa mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbuyuni katika hafla hiyo leo
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa ameketi kwenye meza yake katika ofisi ya waalimu katika shule ya Msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako