Tuesday 16 February 2016

MBWA MWITU HIFADHI YA SERENGETI WAANZA KUONGEZEKA

Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe amepongeza jitihada zinazofanywa na watafiti kwa kurudisha mbwa mwitu katika Hifadhi ya Taifa Serengeti baada ya kutoweka katika miaka ya tisini. Waziri Maghembe alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki alipokuwa akiachia huru kundi la sita la mbwa 11 waliokuwa wamehifadhiwa katika boma maalum ili kurejea katika makazi yao ya asili.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (MB) akiongea wakati wa tukio la kuachia huru kundi la sita la mbwa mwitu 11 waliokuwa wamehifadhiwa kwa miezi sita kwenye boma maalumu la mradi wa mbwa mwitu

No comments:

Post a Comment

Maoni yako