Friday 25 July 2014

AIR ALGERIE YAENDELEZA MACHUNGU YA MAJANGA YA NDEGE

Wakati bado ulimwengu waomboleza vifo vya watu 298 walioangamia kwa kudunguliwa ndege ya Malaysia,na pia ile ajali ya ndege ya Taiwan, Ndege ya Air Algerie aliyoanguka huko Mali ni janga kubwa kwa Afrika na Ulimwengu. Watu wote 116 waliokuwa katika ndege hiyo wamepoteza maisha jangwani.Ndege hiyo ilikuwa safarini kutoka BurkinaFaso kwenda Algeria.
Hii ni mojawapo ya ndege ya shirika la Air Algerie
Mabaki ya ndege hiyo iliyoanguka Jangwani na kuungua. Inasemekana Majeshi ya Ufaransa yalotumwa kuitafuta ndege hiyo yamefanikiwa kupata kinasa sauti na matukio ya ndege hiyo (Black Box). Wengi wa waliopoteza maisha katika ndege hiyo ni raia wa Ufaransa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako