Sunday 22 February 2015

TULIPOTOKA NA TULIPO: USAFIRI WA NDEGE TANZANIA


Boeing 737-2R8C Iliyopewa jina Kilimanjaro ikiwa katika huduma mwaka 1978

Boeing 707-320 Iliyopewa jina la "Ngorongoro Crater" ikiwa katika uwanja wa ndege wa Zurich huko Uswisi katika moja ya safari zake mwaka 1980
Boeing 737-236 Baada ya kampuni hiyo kuingia ubia na Shirika la ndege la Afrika ya Kusini na kuzindua ndege hii mwaka 2002
Airbus A320-214.Shirika hilo likaendelea tena kushirikiana na Afrika Kusini lakini kipindi hiki rangi ya ndege zake ikabadilishwa tena
The De Havilland Canada DHC-8Q-311 DASH 8 5H-MWG Baada ya kukumbwa na madeni na matatizo mengine ya ndani ya Shirika, ATCL ikajikuta inabakiwa na ndege hii ambayo iliingizwa Novemba 2012 kufanya safari za ndani kati ya Dar-Tabora-Kigoma.

Baada ya kufunguliwa kwa Uwanja wa ndege wa Songwe Mbeya, shirika hili limekodisha ndege kutoka Shirika la ndege la Kenya kuhudumia.

NB>:Ila tunachojiuliza imekuwaje maana Shirika hili miaka ya 70 na 80 ilikuwa inatoa huduma nzuri sana za ndani na nje ikihudumia kutoka Dar es Salaam to Athens (707),
Antanarivo (737), Bombay (707) Bujumbura (737, Cairo (707), Frankfurt (707), Kigali (737), London-xx Gatwick (707), Mahe(737), Maputo (737), Mauritius (737), Moroni (FKF), Muscat (737) and Rome (707).
Nembo na rangi vimebadilika nadhani kwa mawazo yangu ya zamani iliwakilisha vizuri Tanzania kuliko sasa

No comments:

Post a Comment

Maoni yako