Friday 6 February 2015

TANZANIA KUBADILISHANA WAFUNGWA NA NCHI ZA MAURITIUS NA THAILAND

SERIKALI ya Tanzania imeingia mkataba wa kubadilishana wafungwa kwa nchi za Thailand na Mauritius ambapo hadi sasa Tanzania imeweza kupokea wafungwa kumi kutoka nchi hizo kutekeleza mkataba huo.
Hayo yameelezw a na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Pereira Silima alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Ritta Kabati aliyetaka kujua u ni nchi zipi Tanzania imesainiana nazo mkataba wa kubadilishana wafungwa.
Naibu Waziri Silima aliongeza kuwa katika kutekeleza mkataba kati ya wafungwa hao 10, tisa wameshamaliza hukumu za vifungo vyao huku mmoja anategemea kumaliza kutumikia kifungo mwaka 2021.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako