Tuesday 7 July 2009

MALI ASILIA NA MISIMU YAKE

Nyanya na viazi vyavutia macho kweli kweli. Ni mazao asilia ya nyumbani. Hapa ni maeneo ya Msimbazi Jijini Dar.
Ni msimu wa machungwa na machenza sasa. Nyumbani ni furaha ya kupata juice asilia (Natural/fresh juice). Machungwa na machenza hulimwa kwa wingi wilayani Muheza Tanga. Tujitahidi kula matunda haya mazuri kwa afya yetu. Ushauri huu hutolewa kwa lugha ya kiingereza "A fruit a day, keeps the doctor away", ni namna nyingine ya kusema matunda hutupatia afya na kutuepusha na maradhi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako