Sunday 12 July 2009

AMANI MUHIMU

Katika mazingira anayoishi mtoto huyu amani imetoweka. Ni mtoto mdogo sana lakini analazimika kushika mtutu wa bunduki kujilinda au kutetea amani. Si sahihi, viongozi wanapaswa kuwa makini kwa hili maana halitoi mwelekeo mzuri
Tanzania tunajivunia kuwa na amani. Hii ni tunu ambayo tunatakiwa kuilinda. Watoto hawa japo mazingira yaonekana kama ya tabu kidogo lakini wana amani. Tuiendeleze amani iliyopo.
Niitazamapo picha hii pia napata ujumbe kuwa wapo katika mazingira yenye amani ndio maana wapo katika hali hiyo, lakini pia ni muhimu Kujiuliza;hapo wameenda kufanya nini? na je wanakifuatilia? Sidhani kama kwa namna hii tunaweza kuendeleza Amani tuliyonayo maana haioneshi kama kuna ushirikiano katika kujadili au kufuatilia yanayotukabili katika kuimarisha maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na kuimarisha amani.CHANGAMOTO!!!

No comments:

Post a Comment

Maoni yako