Thursday 14 April 2016

JENGO LA "MACHINGA COMPLEX" DAR LAKABIDHIWA MKUU WA MKOA

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene amevunja bodi ya Soko la Machinga Complex lililopo Ilala Mchikini Dar es Salaam na kulikabidhi kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.

Akizungumza leo katika mkutano wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini (JWT), Simbachawene amesema wazo la kuanzishwa kwa soko hilo lilikuwa zuri lakini Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeshindwa kulitekeleza.

Jengo hilo lilikamilika kujengwa mwaka 2010 likiwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 4206, lakini Waziri Simbachawene alisema limeishia kuwa makazi ya popo

No comments:

Post a Comment

Maoni yako