Monday 21 March 2016

MHE DK MOHAMED SHEIN ATANGAZWA MSHINDI KURA ZA URAIS ZANZIBAR

March 20 2016 ilikuwa ni siku ya ambayo Wananchi wa Zanzibar walipata fursa ya kupiga kura ili kuwachagua viongozi wao, na hii ni baada ya kufutwa kwa uchaguzi wa awali uliofanyika october 25 2016.
Leo March 21 Tume ya Uchaguzui Zanzzibar imetangaza matokeo ya uchaguzi huo ambapo imemtangaza mgombea wa CCM Dk Ali Mohamed Shein kuwa Rais Mteule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuibuka na ushindi wa asilimia 91.4%
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa kipindi cha pili cha Uongozi kupitia CCM akipokea cheti maalum cha Ushindi wa Uchaguzi wa marudio kutoka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jecha Salim Jecha wakati wa utoaji wa matokeo ya uchaguzi huo yaliyotolewa jana katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako