Wednesday 20 July 2016

USHOGA TANZANIA HAUKUBALIKI ASEMA MHE RC MAKONDA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam mhe Paul Makonda
DAR ES SALAAM: Watu tisa wanaodaiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja (mashoga), wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni wakituhumiwa kukusanyika kinyume cha sheria kwa lengo la kupinga amri ya Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda ya kupiga marufuku vitendo vya mapenzi ya jinsia moja jijini hapa.Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, watu hao walikamatwa baada ya polisi kuvamia kwenye Ukumbi wa baa ya Matema uliopo Kinondoni B ambako zaidi ya wanaume 200 wanaodaiwa kuwa mashoga, walikusanyika kwa lengo la kujadiliana kwa kina kuhusu amri ya Makonda ya kuwapiga marufuku ili kutoa tamko la pamoja.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako