Monday 11 July 2016

GARI ALILOTENGENEZA KIJANA MBUNIFU WA KITANZANIA JIJINI DAR

Gari aina ya Kaparata lililobuniwa na kijana mtanzania kutoka Gongo la Mboto Dar es Slaam Jacob Louis Kaparata (38).

Akizungumza wakati wa maonyesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam, Kaparata ameeleza kuwa alitumia vifaa vingi vinavyopatikana hapa nchi kuunda gari hilo na kuwa miongoni mwa vitu hivyo vingine alivitengeneza mwenyewe na vingine alichukua vya aina nyingine ya magari.

Chassis nimeitengeneza kwa kutumia square pipe, bodi nimelisuka kwa kutumia brake pipes zinazotumika kutengenezea vitanda na nikatumia mabati ya gauge 18 ambayo yanatumika kutengenezea mageti,” alisema Kaparata.

Injini, diff, gear box na matairi, vyote ni vya gari aina ya Suzuki Carry. Na nimelitengeneza kwa muda wa miezi mitatu na limenigharimu kiasi cha TZS 12,850,000.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako