Sunday 10 July 2016

SHABIKI WA MWENDOKASI WA HAPA KAZI TU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli hivi karibuni katika ziara zake alikutana na kijana aliyemshangilia kwa nguvu zake zote hali ambayo ilimfanya mkuu huyo wa nchi kumwita na kupiga naye picha.
Kijana huyo ambaye anaitwa Omar Abdalah Ramadhani ‘Mkereketwa wa Mwendokasi’ alisikika akisema “Magufuli kule aliko, aminia mzazi, Mungu akupe baraka zote mzazi, na asiyekupenda Mungu atamtokomeza, Watanzania tuko nyuma yako” kauli iliyomfanya Rais Magufuli amwite ili apige naye picha na baadaye kuombewa dua na kijana huyo.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako