Monday 11 July 2016

WAZIRI MKUU WA UINGEREZA KUPATA MRITHI BAADA YA KUJIUZULU JTANO HII

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron amesema kuwa Theresa May atakuwa waziri mkuu wa nchini hiyo baada ya yeye kuachia madaraka jumatano jioni

Theresa May ambaye alikuwa akipigia chapuo nchi hiyo kutojiondoa ndani ya Muungano wa Ulaya atairithi mikoba ya Cameron baada ya yeye kutangaza kuwa ataachia wadhifa huo kufuatia nchi hiyo kupiga kura ya kujitoa katika Muungano wa Ulaya.

May amebakia yeye kutwaa nafasi hiyo baada ya mwanasiasa Andrea Leadsom kujiweka pembeni kwa madai kuwa Uingereza inataka kiongozi imara na anaamini kuwa May anaweza kazi hiyo.
Waziri Cameron atahudhuria mkutano wa mwisho wa baraza siku ya Jumanne na atajibu maswali siku ya Jumatano asubuhi na jioni atakabidhi barua yake ya kujiuzulu kwa Malkia.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako