Friday 22 July 2016

SHAMBULIO ENEO LA MADUKA (SHOPPING CENTRE) HUKO MUNICH GERMANY

Habari zinazoendelea mpaka muda huu ni kuwa limetokea shambulio katika eneo la Olympia Shopping Centre huko Munich kusini mwa Ujerumani. Inasadikiwa watu wengi wameuawa na wengi kuumia. Tayari Polisi, zimamoto, Msalaba Mwekundu na wahusika wengine wapo eneo la tukio kuokoa. Treni zote za chini ya Ardhi (U-Bahn) zimeshimama kufanya kazi.
tutawaletea taarifa zaidi kadiri tutakavyopokea

No comments:

Post a Comment

Maoni yako