Friday 23 October 2015

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU: BAA NA CLUB ZA USIKU ZAPEWA MSIMAMO

Serikali jijini Dar es Salaam imeagiza baa zote zinazouza pombe mpaka asubuhi kusitisha shughuli hiyo mkesha wa siku ya uchaguzi ili kuimarisha usalama Jumapili ijayo.

Aidha, imesisitiza kwamba kila mwananchi atakayekwenda kupiga kura ahakikishe anarudi nyumbani baada ya shughuli hiyo badala ya kukaa katika vikundi kusubiri matokeo vituoni.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, katika ibada maalum ya kuliombea Taifa amani na mvua, iliyoendeshwa na Askofu Charles Gadi wa Kanisa la Huduma ya Good News for All Ministry, jijini Dar es Salaam juzi.

Askofu Gadi katika maombi yake alisisitiza suala la amani na kumuomba Mwenyezi Mungu alete mvua ili mabwawa yanayozalisha umeme yajae maji nishati ya umeme ipatikane nchini kwa uhakika.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako