Saturday 26 November 2016

RAIS WA ZAMANI WA CUBA; FIDEL CASTRO AFARIKI DUNIA

Rais wa zamani wa Cuba na kiongozi wa mapinduzi ya kikomunisti, Fidel Castro amefariki akiwa na umri wa miaka 90, mdogo wake Raul ametangaza.

Amefariki usiku wa saa nne na dakika 22, kwa mujibu wa Rais Raul Castro.

Fidel Castro aliiongoza Cuba kama nchi ya chama kimoja kwa takriban miaka 50 kabla ya Raul kushika madaraka mwaka 2008.

Mazishi yake yanafanyika Jumamosi hii kwa mwili wake kuchomwa moto. Kutakuwepo na siku kadhaa za maombolezo ya nchi nzima.
Siku chache zilizopita akiwa anaongea na waandishi wa habari walofika kumsalimu aliwatabiria kwamba atakufa siku si nyingi na yawezekana hiyo ndo hotuba yake ya mwisho

No comments:

Post a Comment

Maoni yako