Wednesday 25 November 2015

MILION 90 HAZITOSHI KUNUNUA GARI

Mbunge anayedai leo kuwa milioni 90 hazitoshi kununua gari ya maana kufanyia kazi zake za kibunge, basi, wapiga kura waliomchagua mbunge kama huyo wajihesabu wamekula hasara, ama kwa lugha ya mitaani ' Imekula kwao'.
Mbunge kama huyo atakuwa ameonyesha mawili na kwa wazi ; ama amekosa kabisa sifa ya ubunifu, kwamba hata pale wapiga kura wake wangemkabidhi milioni 50 aende Dar na arudi na gari la wagonjwa jimboni, mbunge kama huyo angewaangusha, au, ni mbunge aliyeingia bungeni kwa kujali zaidi maslahi yake binafsi kuliko kutambua hali halisi za wapiga kura wake. Inasikitisha.
Wakai hayo yakiendelea, picha juu yaonyesha moja ya Gari analotumia mmoja wa maraisi "simple" duniani. Je kwa Milioni 90 Rais huyu angenunua magari mangapi kama hilo pichani?

No comments:

Post a Comment

Maoni yako