Friday 6 November 2015

PICHA: KARIBU RAIS WA AWAMU YA 5 MHE. DK. JOHN POMBE MAGUFULI

Rais Mh. Dk. John Pombe Magufuli akila kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Chande kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mara baada ya kushinda uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni
Mhe.Rais Magufuli akikagua gwaride la heshima
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na wanausalama alipowasili Ikulu mara baada ya Kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe
Magufuli (Katikati) Akiongozana na Mkewe Mama Janet Magufuli
walipowasili Ikulu mara baada ya Kuapishwa kwenye sherehe zilizofanyika
katika uwanja wa Uhuru leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
Viongozi mbalimbali waliohudhuria katika picha ya pamoja
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa awamu ya Pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi na Rais wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu leo Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Maoni yako