Thursday 19 November 2015

MHE.KASSIM MAJALIWA APITISHWA KUWA WAZIRI MKUU WA AWAMU YA TANO WA TANZANIA


WAZIRI Mkuu mteule wa Serikali ya Awamu ya Tano, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amesema hakutegemea nafasi ya jina lake kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushika wadhifa wa nafasi hiyo kubwa katika Serikali.
Alisema Uteuzi huo ulioidhinishwa na Bunge, umedhihirisha imani ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyonayo kwake iliyomwongoza katika kuliwasilisha jina lake Bungeni.
Akizungumza mara baada ya zoezi la uthibitisho wa uteuzi wa jina lake Bungeni Mjini Dodoma (leo), Mhe. Majaliwa ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa alisema kilichopo mbele yake kwa sasa ni kuwatumia Watanzania pasipo kujali itikadi ya vyama vyao.
Aliongeza kuwa mara baada ya kuanza kazi yake atahakikisha anazunguka katika mikoa mbalimbali nchini ili kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili Watanzania na maendeleo yaliyofikiwa katika sehemu mbalimbali.
Aidha Mhe. Majaliwa aliwahakikishia Wabunge ushirikiano wa karibu zaidi katika kupokea ushirikiano ili kuweza kuwaletea maendeleo ya haraka Watanzania.
Awali akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa na Wabunge wa Bunge kwa ajili ya kuidhinisha jina hilo, Msimamizi wa jina hilo ambaye ni Katibu wa Bunge, Thomas Kashilill ah alisema katika uchaguzi huo, Mhe. Majaliwa alipata kura za Ndiyo 258 sawa na asilimia 73.5% ya kura zote.
Aidha Kashilillah alisema kura 91 sawa na asilimia 25% ya kura zote zilisema hapana wakati kura 2 sawa na asilimia 0.06% ya kura zote ziliharibika.
Wakizungumzia uteuzi huo, Wabunge mbalimbali Bunge la Jamhuri ya wamesifu uteuzi waMhe. Kassimu Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kusema ni kiongozi mwadilifu, mchapakazi na asiye na makundi.
Alikotoka ni mbali ni tangu enzi za "Masantula/Santana na Pekosi"

No comments:

Post a Comment

Maoni yako