Thursday 8 May 2014

NIGERIA HAPATOSHI

Kufuatia tukio la hivi karibuni la wasichana zaidi ya 200 kutekwa nchini Nigeria na kutokomea kusikojulikana, Mataifa na watu mbalimbali wameingilia kati harakati za kuwatafuta. Marekani imetuma kikosi maalumu kufanya kazi hiyo na tayari manowari imewasili hapo. Viongozi na watu wengine watetea haki za binadamu wamekuwa wakiendelea kupeperusha mabango yenye maandishi "Bring back our girls"
Mke wa Rais wa Marekani Mhe.Michelle Obama akishika kikaratasi chenye ujumbe dhidi ya utekaji wa wasichana hao.

Msichana mwanaharakati wa haki za kinadada Malala akionyesha ujumbe wa kutaka wasichana hao warudishwe

No comments:

Post a Comment

Maoni yako