Tuesday 18 August 2009

ZOMBE NA WENZAKE SASA HURU


Watuhumiwa wakipanda kwenye gari la Polisi baada ya kuachiwa huru kuepa vurugu za wananchi

Gari lililomchukua Zombe likitoka katika eneo la Mahakama baada ya Mashtaka kufutwa

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam,jana ilitoa hukumu ya kushtusha baada ya kumwaachilia huru aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe na wenzake wanane waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji ya wafanyabiashara watatu na dereva teksi mmoja.

Akisoma hukumu hiyo iliyochukua zaidi ya saa sita, Jaji wa Mahakama ya Rufani,Salum Massati, alisema baada ya kupitia ushahidi na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo, amebaini kuwa serikali imeshindwa kuthibitisha mashitaka hayo

Maelezo haya ni kwa hisani ya Na Happiness Katabazi

No comments:

Post a Comment

Maoni yako