Monday 10 August 2009

NAWATAKIENI WADAU WIKI NJEMA ,PILIKAPILIKA KAMA KAWAIDA;

Ni asubuhi kumekucha, unapofikiria kuwahi kwenye majukumu, kumbuka kuna kasheshe kama hii.Jiandae.
Wakati wengine wanatafuta bahati ya kwenda shule, huyu mtoto mpaka akimbizwe kwa fimbo. Mmm wazazi mna kazi, ila ndio hivyo ni mwanao lazima umwelekeze yatakiwayo. Msikate tamaa wazazi,dunia ya leo ina mambo mengi.

Hawa wanawahi zao shule wakiwa peku wanachojali ni kisomo/elimu. Hongereni na muweke bidii sasa katika masomo sio kulia shida tu.Bidii zenu baadae zitasaidia kupunguza shida zilizopo.

2 comments:

  1. Kaka. Heshima kwako. Hizi taswira ni njema na zinaendana saaaana na kuanza kwa wiki.
    Amani kwako.
    Blessings

    ReplyDelete
  2. Ahsante! binafsi nimeianza wiki kwa kukimbia dakika kama 30 hivi. Hayo mambo ya viboko kazi kwelikweli. Ok nami nakutakia muanzo mzuri wa wiki.

    ReplyDelete

Maoni yako