Sunday 31 May 2009

YATIA HURUMA NA KUHAMASISHA VILEVILE

Kila mara nitazamapo picha kama hizi nakumbuka jinsi Tanzania tulivyobarikiwa na maliasili nyingi. Ufisadi umekuwa ni tatizo kubwa. Hali kama hii isingepaswa kuwepo kama Serikali yetu ingekuwa makini. Cheche za Kasi Mpya, Nguvu Mpya na Hari mpya zahitajika sana kubadili hali hii. Angalia watoto wazuri wanavyojitahidi,japo katika hali mbaya hata viatu miguuni hakuna.Serikali inapaswa kuona hili na kuwapa shime kupunguza makali haya.