Sunday 17 May 2009

TANZANIA ASSOCIATION - READING


Tanzania Association Reading
Ndugu Watanzania,

Uongozi wa muda wa Umoja wa Watanzania Reading (Tanzania Association Reading) Unapenda kuwatangazia mkutano wa Watanzania wote wa Reading, Berkshire UK, utakaofanyika tarehe 24th May 2009, Community center, Colley Park,140 Winsley road , RG1 6DW, Reading; kuanzia saa tisa mchana hadi saa mbili jioni (3pm – 8pm), vivywaji na vitafunwa vitakuwepo.

Mkutano huu ni muhimu sana kwetu sisi watanzania wa Reading kwa maana utazungumzia yafuatayo:-

a) Uongozi kutoa taarifa ya maendeleo ya ukamilishwaji wa uundaji wa Umoja huu, na taratibu zake hapa Reading.

b) Kupata taaarifa ya ukamilishwaji wa usajili wa Umoja huu, katika vyombo vya dola hapa Reading.

c) Kuiainisha na kuipitisha katiba, na viambatanisho vyake vya Umoja wa Watanzania Reading.

d) Kuelezea umuhimu wa Umoja wa Watanzania Reading na shughuli zake katika kuboresha maisha ya Watanzania hapa Reading na vitongoji vyake.

e) Kupata maoni, marekebisho na ushauri kuhusiana na vipengele a,b,c) hapo juu.

f) Kutoa mapendekezo na kupanga tarehe ya uchaguzi na utaratibu mzima wa uchaguzi wa viongozi wa kwanza wa kudumu wa Umoja huu hapa Reading vitongoji vyake.

g) Kelezea umuhimu wa kujiunga kuwa mwanajumuia hai wa Umoja huu na faida za kuwa mwanajumuiya hai, na maana yake ni nini.

h) Mengineyo

i) Kuweka action plan na majukumu

j)Email ya jumuiya kwa mawasiliano zaidi ni hii tzra2009@googlemail.com

Kufika kwako ndio kufanikisha mkutano huu na maendeleo yetu hapa Reading.

Kwa mawasiliano zaidi tafadhali wasiliana na

Mwenyekiti wa muda (H.Chang’a) 07954563709

Makamu mwenyekiti (B. Chisumo) 07876126862

Katibu wa muda (S. K. Buraganya) 07894547323

Katibu(Msaidizi) (PeteR Michael) 07888841971



Asante

TA reading

No comments:

Post a Comment

Maoni yako