Tuesday 18 August 2015

KIKOSI KAZI CHA KAMPENI ZA URAIS CCM 2015

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa jana Agosti 17, 2015 katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dokta Jakaya Mrisho Kikwete imekamilisha kazi ya uteuzi wa Wagombea Ubunge katika majimbo mawili ya Singida Mashariki na Kiteto.

Wagombea ubunge walioteuliwa kupeperusha bendera ya CCM katika majimbo hayo ni pamoja na Ndugu Jonathan Njau (Singida Mashariki) na Ndugu Emmanuel Papian John (Kiteto).

Aidha Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Kamati ya Kampeni kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ambayo itaongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. Wajumbe wa Kamati hiyo ni kama ifuatavyo;-

KAMATI YA KAMPENI YA CHAMA CHA MAPINDUZI
Ndugu Abdulrahman Kinana – Mwenyekiti
Ndugu Rajab Luhwavi – Makamu Mwenyekiti – Bara
Ndugu Vuai Ali Vuai – Makamu Mwenyekiti – Z’bar
Ndugu Sofia Simba
Ndugu Mohamed Seif Khatib
Ndugu Asha-Rose Migiro
Ndugu Samwel Sitta
Ndugu Nape Nnauye
Ndugu Mwigulu Nchemba
Ndugu Harrison Mwakyembe
Ndugu January Makamba
Ndugu Amina Makillagi
Ndugu Christopher Ole Sendeka
Ndugu Stephen Wasira
Ndugu Abdallah Bulembo
Ndugu Hadija Aboud
Ndugu Mohamed Aboud
Ndugu Lazaro Nyalandu
Ndugu Issa Haji Ussi
Ndugu Waride Bakari Jabu
Ndugu Mahmoud Thabit Kombo
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha
Ndugu Maua Daftari
Ndugu Stephen Masele
Ndugu Pindi Chana
Ndugu Shaka Shaka
Ndugu Makongoro Nyerere
Ndugu Bernard Membe
Ndugu Sadifa Juma Khamis
Ndugu Antony Diallo
Ndugu Livingston Lusinde
32 . Ndugu Ummy Mwalimu

Imetolewa na:-

Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,

ITIKADI NA UENEZI
18/08/2015

No comments:

Post a Comment

Maoni yako