Saturday 8 August 2015

GESI KUSAFIRISHWA KWENDA DAR WIKI CHACHE ZIJAZO

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC), James Mataragio amesema kuwa gesi asilia itaanza kusafirishwa kwa njia ya bomba kutoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam, baada ya siku wiki mbili kuanzia sasa.
Mataragio ametoa kauli hiyo jana baada ya kutembelea kiwanda cha kuchakata gesi kilichopo kijiji cha Madimba Wilaya ya Mtwara mkoani hapa na kujionea sehemu kubwa ya mradi huo, ukiwa umekamilika kwa asilimia 100.
Hivi karibuni Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alisema umeme wa gesi utaanza kutumika mwezi ujao baada ya ujenzi wa bomba la kupitisha gesi hiyo kukamilika

No comments:

Post a Comment

Maoni yako