Friday 27 December 2013

VIOJA KWENYE DALADALA

Wadau bila shaka mlikuwa na xmasi njema. Sasa tunarudi tena kwenye majukumu kabla ya kufunga mwaka. Lakini tujikumbushe vioja hivi tunavyokumbana navyo kila siku.


Mlokole: "Nyimbo gani mnapiga?!?
Wekeni nyimbo za Yesu.."
Konda: "Vipi wewe, Yesu bado
hajatoa album...

Abiria: "Kuna Kiti au unasema
panda tu!?"
Konda: "hao wengine wamekalia
ndoo?! "

Abiria: "Embu punguzeni sauti ya
redio..."
Konda: "Sheria za nchi tu
zinatushinda, tusikilize na zako!?
hebu tupunguzie misheria"

Mmama: "Bwana ondoa gari joto
sana!!"
Konda: "Usituzingue wewe,
shuka upande fridge...."

Konda: "Anti, kuna siti pale
nyuma,ingia...."
Anti: "Siwezi kaa siti za nyuma..."
Konda: "Kwani za nyuma ziko nje ya gari?!"

Sister duu: "Konda unanibana
bwana..."
Konda: "mbona nguo ulizovaa
huzisemi, kama ulitaka kujiachia
ungekodi treni peke yako

Sharobaro: "Kuna kiti?! Kama
hamna sipandi..."
Konda: "Kama unaogopa kukosa
kiti si ungebeba chako!!?"

No comments:

Post a Comment

Maoni yako