Friday 20 December 2013

BREAKING NEWS:MAWAZIRI 4 KUTENGULIWA VYEO VYAO

 Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda amesema kwamba Rais Kikwete amekubali kutengua nyadhifa za mawaziri wanne kufuatia ripoti ya 'Operesheni Tokomeza' iliyotolewa mapema leo bungeni.  Mawaziri hao waliotenguliwa nyadhifa zao ni: Mhe. David Mathayo David wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Khamis Kagasheki wa Maliasili na Utalii, Mhe. Emmanuel Nchimbi wa Mambo ya Ndani na Mhe. Shamsi Vuai Nahodha wa Ulinzi.  Mhe. Kagasheki alitangaza kujiuzulu mapema kabla uamuzi huo uliotangazwa na Waziri Mkuu. Waziri wa Maliasili na Utalii: mhe. kagasheki Waziri wa Mifugo na Uvuvi:mhe. David Matayo David Waziri wa Mambo ya Ndani mhe. Emanuel Nchimbi Waziri wa Ulinzi na JKT mhe. Shamsi Vuai Nahodha

1 comment:

Maoni yako